Sunday, May 31, 2015

BOKO HARAMU LAUWA WATU 29

Nigeria:Watu 29 wauawa msikitini

Watu 29 wameuawa katikati ya  mji mkuu wa jimbo la Borno Maiduguri Kaskazini Mashariki mwa Nigeria baada ya mlipuaji wa kujitoa mhanga kujilipua ndani ya msikiti.
Kamishna wa polisi katika jimbo la Borno amesema kuwa watu wengine 28 walijeruhiwa kwenye shambulizi hilo.
Shambulizi hilo lilifuatia jaribio la awali la kuuteka ya mji wa Maiduguri lililondeshwa na wanamgambo  wa Boko Haram.
Wanagamabo hao walifyatua makombora kwenye makazi ya watu na kuua takriban watu 13.

MAFURIKO MIKANJUNI ,TANGA

Zaidi ya falimia 11 mtaa wa Mikanjuni A kata ya Mabawa Tanga hazina mahala pa kuishi baada ya nyumba zao kuzingirwa  na maji baada ya mvua iliyonyesha kwa siku mbili mfululizo.
Kujaa kwa maji hayo pia imedaiwa kusababishwa na kutokuwepo kwa miundombinu ya kupitisha maji na hivyo kuwa sababu ya maji kuingia majumbani.
Wakizungumza na tangakumekuchablog mapema leo, wakazi hao walisema kwa muda mrefu wamekuwa wakiwaeleza viongozi juu ya kero hiyo lakini hakuna jitihada zozote zinazochukuliwa.

 Wakazi wa mtaa wa  Mikanjuni A kata ya Mabawa Tanga, wakiangalia nyumba iliyozingirwa na maji baada ya mvua kubwa kunyesha kwa siku mbili mfululizo ambapo jumla ya familia 11 hazina pahala pakuishi. Maji hayo hayana njia za kupita baada ya kutokuwepo kwa miundombinu ya mifereji ya kupitisha maji.


Kwa habari, matukio na burudani ni hapa hapa tangakumekuchablog

FERDINAND ATUNDIKWA MADALUGA

Kauli ya Rio Ferdinand na hatma ya soka lake..

yeye
Akiwa bado kwenye majonzi makubwa ya mkewe aliyefariki duniani mwanzoni mwa mwezi huu, beki wa zamani wa Manchester United na timu ya Taifa ya England Rio Ferdinand ameweka wazi mikakati yake mipya katika mahojiano aliyoyafanya.
Mchezaji huyo ambaye kwa sasa ana miaka 36 ametangaza nia ya kustaafu soka baada ya klabu ya Queens Park Rangers kutangaza kumtema kwenye kikosi chake.
na mkewe
Rio Ferdinand akiwa na marehemu mkewe Rebecca
Alitangaza uamuzi wake katika mahojiano ya moja kwa moja na BT Sport, na aliandika kwenye akaunti yake ya Twitter kuwashukuru waliomtakia kila la heri baada ya kifo cha mkewe, Rebecca aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi ya saratani, ambaye wamezaa naye watoto watatu.
Ferdinand hakuacha kumsifia kocha wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson kwamba ni mfano wa kuigwa kutokana na ujuzi wake.
Manchester United ilitoa Pauni Milioni 30 kumnunua Ferdinand Julai mwaka 2002 na kumfanya awe beki ghali katika historia ya soka ya Uingereza wakati akisajiliwa kutoka Leeds United.
Unahitaji cho
Kwa habari, matukio na burudani, ni hapa hapa tangakumekuchablog

ALIPANDIKIZWA USO WA MAREHEMU BAADA YA KUPATA AJALI MBAYA

Jana tuliweka post hii ya Richard Norris aliepata ajali na kuwekwa uso wa marehemu na leo nimekuwekea mwendelezo wa tukio hilo ambalo limekuwa gumzo kwa washabiki wa blog hii

dada
Ajali nyingi duniani zimekua zikisababisha vifo vya watu wengi huku zikiacha wengine wakiwa na ulemavu wa maisha ambao huwasababishia kupoteza mwelekeo wa maisha yao na kukata tamaa kabisa.
Pamoja na wengi kubaki na ulemavu, lakini pia madaktari wamekuwa kijitahidi kadri wawezavyo kuwarudisha watu hao katika hali zao lakini moja ya tukio la kushangaza ni la kijana Richard Norris ambaye alipata ajali mbaya na kumpelekea kuharibika vibaya sura yake.
ajali
Picha ikimwonyesha Norris kabla hajapata ajali, alivyopata ajali na baada ya kuwekewa uso mwingine wa marehemu
Unaambiwa baada ya ajali hiyo kijana huyo alishindwa kutoka nyumbani kwa takribani miaka 15 na amini usiamini kijana huyo alifanyiwa upasuaji wa kihistoria uliochukua masaa 36 na kupandikizwa uso mpya wa mtu ambaye alishafariki baada ya kupata ajali.
Upasuaji huo ulifanyika katika hospitali ya University of Maryland Medical Center na ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa na sasa kijana huyo anaendelea vyema akiwa mwenye furaha.
sura
Mwonekano wa Norris baada ya Baada ya upasuaji
Kwa kawaida kwa sababu ya maadili ya utabibu watu waliopewa mabaki ya viungo vya wafu hawaruhusiwi kukutana na jamaa au ndugu wa marehemu, lakini Norris hakuweza kujizuia kukutana na Aversano, kutoka Maryland ambaye ni dada wa marehemu.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapa hapa tangakumekuchablog

SOMA MAKUBWA YALIYOANDIKWA NA MAGAZETI YA LEO, MAY 31 TZ

Uchambuzi huu wa magazeti unaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya kituo cha Elimu Cha Candle Education Centre Tanga, kituo kinaongoza kufaulisha wanafunzi kidato cha pili hadi cha sita na wale wanaojiendeleza kielimu. Kituo kimesajiliwa na NECTA  na kiko na Hostel. Wapo Tanga mkabala na Bank ya CRDB simu, 0715 772746

J2MWANANCHI
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Ngoyai Lowassa amesema ana ari, shauku na uwezo wa kuongoza Taifa wakati alipotangaza nia yake ya kugombea urais kwa tiketi ya CCM katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na maelfu ya watu kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.
Lowassa, ambaye ni mbunge wa Monduli akihutubia maelfu ya wakazi wa Arusha, katika Uwanja a Sheikh Amri Abeid Aluta, alisema ameamua kujitokeza tena kuwania urasi kwa kuwa anaamini yeye ndiye mtu sahihi wa kuiongoza nchi wakati huu.
Zaidi ya watu 30,000 walifurika kwenye uwanja huo wakiwa wamekaa kwenye viti na wengine ndani ya kiwanja cha mpira huku, mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombare Mwiru akiongoza mlolongo wa watu mashuhuri waliojitokeza kumuunga mkono mbunge huyo wa Monduli katika mbio za kuelekea Ikulu anazoziita “safari ya Matumaini”.
Akihutubia mkutano huo, Lowassa alisema pamoja na kuwa viongozi waliopita wameliongoza taifa hili vizuri, bado linahitaji kiongozi mwenye uthubutu na uongozi madhubuti unaoweza kufanya maamuzi magumu.
“Kuamini kama una uwezo na shauku, hakuna budi kwenda sambamba na uwezo wa kusimamia yale unayoyaamini. Na kwangu haya mawili ni dhahiri. Nina ari, nina shauku na nina uwezo, kama rekodi yangu inavyothibitisha,” alisema Lowassa huku akishangiliwa.
“Tunapomtafuta Rais wa Jamhuri ya Muungano ni lazima tukumbuke kwamba tunamtafuta mtu ambaye atakuwa pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama katika nchi yetu. Na kwa Chama cha Mapinduzi tunamtafuta mtu ambaye atakuwa pia mwenyekiti wa chama chetu.
“Naamini kwa vigezo vyote, nina kila sifa ya kubeba dhamana hizo nzito. Katika mambo ambayo najivunia, na sitayasahau katika historia yangu ni kushiriki kwangu kuilinda nchi yetu pale nilipohitajika. Nilishiriki kikamilifu katika Vita vya Kagera nikiwa miongoni mwa askari wa mstari wa mbele wa mapambano.”
Lowassa pia alikumbusha tukio la mwaka 1995 alipojitokeza kugombea urais kwa pamoja na Rais Jakaya Kikwete.
“Natarajia safari hii, Kikwete ataniunga mkono.”
Hata hivyo, Kikwete hakupitishwa na CCM mwaka huo na akagombea peke yake 2005, mwaka ambao Lowassa alisema aliamua kwa dhati kumuunga mkono mwenzake.
MWANANCHI
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema uandikishaji wa wananchi kwenye Daftari la Wapigakura nchini utamalizika mwishoni wa mwezi ujao baada ya mashine 1,600 zaidi za kielektroniki kwa ajili ya kazi hiyo kuwasili juzi.
Ofisa ugavi mwandamizi wa NEC, Datus Matuma alisema mashine hizo zinazotumia teknolojia ya utambuzi wa alama za mpigakura (Biometric Voter’s Registration), zitaanza kupelekwa mikoa ya Mara, Arusha, Manyara na Kilimanjaro.
“Ule uvumi ambao ulikuwa ukienea nchini kwamba Tume ya Taifa haiwezi kumaliza uandikishaji, sasa umefikia mwisho kwani hizi mashine ni za kisasa na zitaanza kazi moja kwa moja kwenye mikoa hiyo niliyoitaja na mwishoni mwa mwezi Juni au mwanzoni mwa mwezi wa Julai watu wote watakuwa wameshaandikishwa,” Matuma.
Alisema wananchi wajitokeze kwa wingi kujiandikisha ili wasikose haki yao ya msingi ya kupiga kura kwani kila aliyefikisha umri wa kupiga kura anatakiwa kujiorodhesha kwenye daftari hilo.
Alisema Serikali ni sikivu ndio maana imekata kiu ya Watanzania kwa kuleta mashine hizo ambazo sasa zimefikia 8,000 na zinakidhi kabisa mahitaji ya Watanzania wote kwani zinafika kila mkoa na zitagawiwa kwenye halmashauri kwa ajili ya kuzisambaza kwenye vituo vya uandikishaji .
Hata hivyo, mwezi uliopita NEC ilitangaza kwamba hakuna mpango wowote wa kuahirisha Uchaguzi Mkuu na kusisitiza kuwa utafanyika kama ilivyopangwa.
MWANANCHI
Mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi jana uligeuka shubiri kwa Waziri Samuel Sitta wakati alipobanwa na wabunge kutokana na Serikali kushindwa kuboresha usafiri wa reli na anga.
Wabunge hao, mbali na kuibua ufisadi mbalimbali unaofanywa na watendaji wa Serikali, wakiwamo wa wizara hiyo, walihoji sababu za Serikali kuwa na ndege moja tu na kushindwa na nchi ndogo ya Rwanda ambayo ina ndege saba za serikali.
Licha ya kuipitisha, walisema kuwa nchi bila kuwa na usafiri unaoeleweka wa reli, anga na barabara ni vigumu kupata maendeleo.
Akichangia mjadala huo, mbunge wa Kawe, (Chadema), Halima Mdee aliibua suala la ukiukwaji wa mauzo ya nyumba za Shirika la Reli Tanzania na Zambia (Tazara), kwamba mbali na ukiukwaji wa mauziano na ununuzi, pia mfanyabiashara aliyenunua nyumba hizo amekwepa kodi ya Serikali inayokadiriwa kufikia Sh4 bilioni
Haiwezekani, tuna taarifa hizo, nyumba zimeuzwa kwa bei ya soko na Serikali pia ilipaswa kupata kodi yake inayofikia wastani wa Sh4 bilioni… Serikali hii ni ya aina gani ambayo kila mwaka kuna kashfa za ufisadi katika wizara zake,”  Mdee.
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, alisema katika serikali ya Awamu ya Nne kila wizara inakabiliwa na wizi, akifafanua jinsi Mamlaka ya Manunuzi Nchini (PPRA) ilivyoshindwa kufuata vigezo ya ununuzi wa mabehewa 124 ya Kampuni ya Reli (TRL).
Alivitaja vigezo hivyo kuwa ni pamoja na utangazaji wa zabuni kutozingatiwa na pia kutofanyika kwa uchunguzi.
Alisema waziri wa uchukuzi na katibu mkuu wa wizara hiyo na waziri wa fedha ambao ndio waidhinishaji wa fedha hizo za ununuzi wa mabehewa wanatakiwa kuwajibika. Alisema suala hilo linalohusu Sh230 bilioni haliwezi kufunikwa na kupita.
Alisema Rwanda ni nchi ndogo lakini ina ndege saba wakati Tanzania ni nchi kubwa lakini ina ndege mmoja tena inahitaji matengenezo kila siku.
MWANANCHI
Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na usalama Wilayani Bukombe Amani Mwenegoha amesematangu kutokea kwa mauaji ya mtoto albino Yohana Bahati Wilayani Chato, kumeibuka madai mbalimbali ya utapeli na vitisho vinavyofanywa na watu wenye ulemavu huo.
Mwenegoha alisema kuna utapeli unadaiwa kufanywa na wasichana wenye ulemavu wa ngozi wanaofanya biashara ya kujiuza miili yao Wilayani humo.
Imedaiwa kuwa wasichana hao huwageuka wanaume wanapofika kwenye nyumba za kulala wageni licha ya kukubaliana toka awali.
Kuna taarifa ambazo zimetufikia ofisini kwetu kwamba hawa wasichana wanasimama barabarani sehemu za vichochoro wakiona wanaume wakawapenda wanawaita na kuwalazimisha wawape fedha, wakikataa wanapiga kelele na kudai kuwa wanataka kuwakata viungo vyao”Mwenegoha.
Pia wanapokuwa kwenye biashara yao ya kujiuza wanapokutana na wanaume hukubaliana kiwango cha fedha, lakini wanapofika ndani hubadilika na kuwalazimisha watoe fedha zaidi ya makubaliano na wakikataa kuwa wanataka kukatwa viungo.
NIPASHE
Watu wawili wamefariki dunia mkoani Simiyu katika matukio tofauti akiwamo mtoto wa miezi mitatu aliyenyakuliwa na fisi akiwa mgogoni mwa mama  yake.
Kamanda wa Polisi  wa  mkoa wa Simiyu, Gemin Mushy  jana alisema  kuwa mtoto Ng’wanza Samwel, akiwa amebebwa na  mama  yake alinyakuliwa na fisi Mei 25, majira ya saa 1;30 jioni katika kijiji cha Ngugunu,Tarafa ya Kisesa wilayani Meatu.
Alisema katika kufuatilia tukio hilo, mabaki ya mtoto huyo yalipatikana mita 200 tu fisi kutoka eneo alilonyakuliwa huku kichwa, kifua, tumbo, mikono na miguu  ikiwa haipo.
Katika tukio jingine mpanda baiskeli aliyefahamika kwa jina la Magina Supa(20), mkazi wa Nyaumata mtaa wa Kisiwani wilayani Bariadi, aliuawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali shingoni na bega la kushoto na mtu aliyekuwa amempakiza kama abiria wake.
Akifafanua, Kamanda  Mushy alisema kuwa tukio  hilo lilitokea Mei 26 majira saa 1;00 jioni katika mtaa wa Izunya, kata ya Somanda tarafa ya Ntuzu wilayani Bariadi kwa mtuhumiwa wa mauaji hayo anayedaiwa kuwa abiria wa mpanda baiskeli huyo aliyekuwa  anajishughulisha na biashara ya daladala ya baiskeli.
Kamanda huyo alisema kuwa mara  baada ya mauaji hayo, mtuhumiwa ambaye hajafahamika na anasakwa baada uhalifu huo alitoroka. Chanzo cha mauaji hayo  hakijafahamika.
NIPASHE
Walemavu wa aina mbalimbali karibu milioni nne huenda wasipige kura kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu kutokana na kukosekana vifaa vya kuwawezesha kushiriki  zoezi hilo.
Baadhi ya vifaa hivyo ni kama maandishi ya nukta nundu kwa wasioona,  hadi sasa  havijanunuliwa.
Kamishna wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), Jaji Mstaafu John Mkwawa, alisema  matarajio ya kupatikana kwa vifaa hivyo yanasubiri kufunguliwa zabuni katikati ya mwezi ujao.
Alitoa maelezo hayo  baada ya kuulizwa iwapo  Nec ina vifaa vya kuwasaidia walemavu hao na kama wamepewa elimu kuhusu matumizi ya  vifaa hivyo, kwa vile mwaka 2010 walilalamikia ukosefu wa elimu na vifaa vya kuwawezesha kushirika zoezi hilo.
Jaji Mkwawa alisema jitihada zinafanywa na tangazo la kutafuta wazabuni wa kuagiza vifaa hivyo lilitolewa Mei 12, mwaka huu kwenye vyombo vya habari.
Alisema idadi ya walemavu wenye sifa za kupiga kura mwaka huu ni milioni nne hivyo Nec  haipo tayari kuwakosesha haki wananchi hao.
Kuhusu suala la utoaji wa elimu kwa watu hao ambalo mwaka 2010 walilikosa, Jaji Mkwawa aliahidi kueleza zaidi taarifa hizo kabla ya kupatikana vifaa hivyo.
Hata hivyo, alipoulizwa idadi ya vifaa wanavyokusudia kuviagiza, Jaji Mkwawa alisema  ni mapema kulielezea kabla ya zabuni kufunguliwa.
NIPASHE
Hatima ya Mpango wa Taifa wa Damu Salama (NBTS) upo kwenye hati hati  baada ya mfadhili mkuu aliyekuwa anagharamia uendeshaji wake kuondoka rasmi leo na kuiacha ikichechemea.
Serikali ya Marekani kupitia kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC), ilikuwa akigharamia sehemu kubwa ya mishahara ya wafanyakazi, vifaa vya kuhifadhia na kusafirishia damu.
Uchunguzi wa umebaini kuwa, NBTS ina hali mbaya kwa vile mafadhili anaiacha  wakati benki hiyo  inakabiliwa na uhaba wa damu ambayo ni tegemeo kwa  wagonjwa waliopo mahospitalini hasa wanawake wajawazito, wazazi na watoto wachanga.
Msemaji wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Nsachris Mwamwaja, alikiri kujitoa kwa mfadhili huyo na kuongeza kuwa, serikali imejipanga kukabiliana na changamoto hiyo ikiwa ni pamoja kubeba mzigo wote wa ulipaji mishahara kwa wafanyakazi na kuhakikisha  damu na vifaa vinavyohitajika vinakuwepo wakati wote.
“Tunatambua umuhimu wa damu kwa wagonjwa, hata bajeti yetu itakayowasilishwa keshokutwa bungeni tutalitilia mkazo suala hili kwa sababu mfadhili huyu alikuwa anatusaidia na sasa amejitoa hivyo hatuna jinsi,”.
Kuhusu uhaba wa damu, aliwataka Watanzania kujitokeza kuchangia damu kwa sababu mahitaji yake ni makubwa na kila mtu anaweza kuhitaji msaada huo.
“Suala la damu halihusiani na mfadhili bali watu wajitolee kwa sababu damu inasaidia kila mtu bila kujali ni nani unacheo gani, niwaombe muwe na utaratibu wa kuchangia damu ili tuokoe maisha ya watoto, wanawake, wanaume, wazee,” alihimiza.
NBTS imekuwa ikitegemewa kusambaza vitenganishi kwenye kanda zake sita ambazo ni Mwanza, Moshi, Tabora, Mbeya, Mtwara na Dar es Salaam.
HABARILEO
Maofisa watano wa Serikali, wanatarajiwa kupandishwa kizimbani hivi karibuni, kutokana na kashfa ya uagizaji wa mabehewa 274 kutoka India, huku wengine wakitarajiwa kuchukuliwa hatua za kiutawala.
Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta, ameliambia Bunge jana kuwa Kamati Maalumu iliyoundwa na wizara yake, imemaliza kazi na kumkabidhi ripoti hiyo.
“Wamenikabidhi ripoti juzi na iliundwa na watu wa Ofisi ya CAG, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Takukuru  na wahandisi,” alisema Sitta.
Alikuwa akifanya majumuisho ya hoja za wabunge kuhusu makadirio ya bajeti yake kwa mwaka wa fedha 2015/16, ambayo aliyawasilisha bungeni jana asubuhi na kupitishwa na Bunge baadaye mchana.
Waziri huyo mkongwe alisema kamati hiyo ilienda hadi Calcutta, India ambako mabehewa hayo 274 yalitengenezwa na kwa mujibu wake, mabehewa hayo si chakavu, kama ilivyodaiwa awali.
Hata hivyo alisema “kuna makosa mawili hapa ambayo ni uzembe wa pande mbili, waagizaji na watengenezaji. Kuna tatizo katika specification (vipimo). “Hapa kuna majina ya watu wote waliohusika katika suala hili.
Watano tunawapeleka mahakamani, wengine tutawachukulia hatua za kiutawala.” Aidha, aliweka bayana kuwa katika maofisa hao watano watakaopelekwa mahakamani, wawili ni wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Aidha, Sitta alisema si kweli kuwa hasara iliyopatikana ni Sh bilioni 200, bali ni Sh bilioni 12 na wote waliohusika watachukuliwa hatua stahili. “Pia tumemwomba Mwanasheria Mkuu ili sehemu ya hasara hii ibebwe na mtengenezaji na nyingine itabebwa na Serikali kutokana na uzembe uliofanyika,” Sitta.
Kwa habari, matukio na burudani ni hapa hapa tangakumekuchablog

AMKA NA MAGAZETI NA TANGAKUMEKUCHABLOG

Magazeti yanaletwa kwenu kwa hisani kubwa ya kituo cha Elimu Cha Candle Education Centre Tanga. Kituo kinaongoza kufaulisha wanafunzi kidato cha pili hadi cha sita na wanaojiendeleza kielimu. Pia wako na Hostel. Wapo Tanga mkabala na Bank ya CRDB simu 0715 7727246

mgUngana na mimi tena kwenye post hii ya Magazeti, post maalum ambayo huwepo hapa tangakumekuchablog kila siku kwa ajili ya kuyasogeza karibu yako Magazeti mbalimbali ya Tanzania na habari zake kubwakubwa kwenye kurasa za mwanzo na mwisho.
DSC03108
DSC03109
DSC03110
DSC03111
DSC03112
DSC03113
DSC03114
DSC03115
DSC03116
DSC03117
DSC03118
DSC03119
DSC03120
DSC03121
DSC03122
DSC03124
DSC03137
DSC03138
DSC03139
DSC03140

DSC03126
DSC03127
DSC03128
DSC03129
DSC03130
DSC03131
DSC03133
DSC03134
DSC03135
DSC03136Kwa habari na matukio usiache kuungana nami hapa hapa tangakumekuchablo

Saturday, May 30, 2015

ALIEPANDIKZWA USO AKUTANA NA DADA WA MAREHEMU

Aliyepandikizwa uso akutana na dadake marehemu

Norris kabla ya operesheni
Mwanamke ambaye kakake alikufa katika ajali mbaya ya barabarani amekutana na mtu aliyepewa uso wake.
Amini usiamini mtu huyo aliyefanyiwa upasuaji huo wa kihistoria alipandikizwa uso mpya baada yake kuishi kwa miaka 15 akiwa bila pua.
 Richard Norris alimshukuru mwanamke huyo kwa niaba ya kakake marehemu aliyemwezesha kupata mwanzo mpya maishani.
Mwanamke huyo Rebekah Aversano alionekana akiugusa uso wa kakake akiwa haamini macho yake.
 Richard Norris, anayetokea Virginia, Marekani alijeruhiwa katika ajali ya ufyatulianaji wa risasi miaka 15 iliyopita.
Yamkini Norris hakuwa amewahi kutoka nyumbani kwake katika kipindi hicho chote.
 
Kwa kawaida kwa sababu ya maadili ya utabibu watu waliopewa mabaki ya viungo vya wafu huwa hawakutani na jamaa za wale waliochangia, lakini Norris hakuweza kujizuia kukutana na bi
Aversano, kutoka Maryland.
Na alipomuona  Aversano, alibubujikwa na machozi na kusikika akisema ''hii ndiyo uso na sura niliyokuwa nayo''
Kakake Joshua Aversano, alipoteza maisha yake katika ajali mbaya ya barabarani akiwa na umri wa miaka 21.
kauli yake ya kutoa viungo vya mwili wake haikupokelewa vyema na familia yake na haswa mamake Gwen Aversano.
''Lakini kwa sababu hilo ndilo alilopenda sisi kama familia yake hatungempuuza'' alisema mamake katika mahojiano na runinga ya CTV.
''Baada ya kukutana na Norris aghalabu nimeweza kumuona mwanangu tena''
''Nahisi vyema kuwa nimemsaidia Norris kuanza upya maisha yake japo tumempoteza mpendwa wetu'' alisema mamake Joshua .
Upasuaji huo wa kihistoria ulifanywa katika chuo kikuu cha Maryland yapata miaka mitatu iliyopita.
Upasuaji ambao ulidumu kwa zaidi ya saa 36.

UJERUMANI NDIO NCHI PEKEE YENYE IDADI NDOGO YA WATOTO DUNIANI

Ujerumani ina idadi ndogo zaidi ya watoto duniani

Idadi ya watoto wanaozaliwa nchini Ujerumani imepungua zaidi ya mataifa yote duniani.
Utafiti umeonesha kuwa idadi ya watoto wanaozaliwa nchini Ujerumani ndiyo ya chini zaidi duniani na sasa kunahofu kuwa kupungua kwa uzazi kutaathiri pakubwa uwezo wa vijana kuendeleza kasi ya ukuaji wa uchumi wa taifa hilo tajiri zaidi barani Ulaya.
Watafiti wanaonya kuwa endapo jitihada mahsusi hazitafanywa ilikuimarisha idadi ya watoto nchini humo basi uchumi wa taifa hilo utaathirika vibaya.
Kulingana na utafiti huo,watoto 8.2 pekee walizaliwa miongoni mwa watu wazima 1000.
Awali idadi ya chini zaidi ilikuwa ya Japan ambayo huandikisha idadi ya watoto 8.4 wanaozaliwa miongoni mwa watu wazima 1000.
.
Kampuni ya uhasibu ya Ujerumani BDO ikishirikiana na chuo cha utafiti wa kiuchumi cha Hamburg Institute of International Economics (HWWI) ndiyo iliyoendesha utafiti huo kwa lengo la kutathmini uwezo wa uchumi wa taifa hilo kujiendesha mbali na viwango vya uzazi vinavyoripotiwa nchini humo.
Barani Ulaya, Ureno na Italia ziliorodheshwa katika nafasi ya tatu na nne zikiwa na jumla ya watoto 9.0 na 9.3 mtawalia.
Ufaransa na Uingereza zinasajili watoto 12.7 wanaozaliwa miongoni mwa watu wazima 1000.
Niger iliyoko Afrika ndiyo inayoandikisha idadi kubwa zaidi ya watoto wanaozaliwa duniani.
Nchini humo watoto 50 huzaliwa miongoni mwa watu wazima 1000.
 
Kulingana na utafiti huo wa BDO iwapo hali itaruhusiwa kuendelea hivyo basi idadi ya watu wenye umri wa kati ya miaka 20 na 65 wenye uwezo wa kufanya kazi na uwezo wa kuendesha uchumi wa taifa hilo itapungua kwa asilimia 61% hadi 54% ifikapo mwaka wa 2030.
Aidha afisa wa BDO Arno Probst, aliwatahadharisha wajerumani kuwa kiwango cha malipo na mishahara ya wafanyikazi kitaongezeka maradufu kadri ya upungufu wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi .
Probst alisema Ujerumani italazimika kuwaruhusu wahamiaji kuingia nchini humo na kufanya kazi ilikuepuka kuzorota kwa uchumi wake.
Hutopitwa na habari na niko tayari kukusogezea muda na wakati kupitia hapa hapa tangakumekuchablog

BLATTER ACHAGULIWA TENA KWA KISHINDO

FIFA:Blatter ailaumu UEFA na Marekani

Rais wa shirikisho la soka duniani FIFA Sepp Blatter ameikashifu shirikisho la soka barani Ulaya UEFA na Marekani kwa kuendesha kampeini ya kuipaka tope jina zuri la FIFA.
Blatter ambaye ameanza muhula wake wa tano kama rais wa shirikisho hilo amesema kuwa alipigwa na mshangao alipopata habari za ufisadi ulaji na rushwa ndani ya FIFA.
Akizungumza na runinga moja ya Uswisi Blatter alimtaja mkuu wa sheria wa Marekani Loretta Lynch na rais wa UEFA Michel Platini kwa kuichukia FIFA.
''Kwa kweli chuki inayosikika katika tuhuma za ufisadi na ulaji rushwa dhidi ya FIFA kwa hakika sio kitu cha kudhaniwa na mtu mmoja hiyo ni chuki ya shirikisho lote la UEFA.
''Lakini mimi nitawasamehe tu '' alisema Blatter.
Blatter alilaumu vyombo vya habari kwa kujaribu kuchochea njama ya kuiharibia FIFA jina.
Blatter alitawazwa rais wa FIFA baada ya kujiondoa kwa mpinzani wake Ali Bin al Hussein mwanamfale wa Jordan baada ya kushindwa katika mkondo wa kwanza wa uchaguzi kwa kura 133 kwa 73.
Blatter, ambaye ameongoza shirikisho hilo kwa miaka 17 amewataka wajumbe wa FIFA kushirikiana na kuwa imara. .
Akifungua mkutano mkuu wa FIFA mjini Zurich, Bwana Mr Blatter alibainisha kuwa shirikisho hilo linakabiliwa na matatizo - lakini akatoa wito kwa wajumbe kushughulikia matatizo hayo kwa pamoja.
Lakini kabla upigaji kura , mpinzani mkuu wa bwana Blatter , Ali Bin al Hussein mwanamfale wa Jordan, aliwaomba wajumbe wa mkutano huo kumuunga mkono -- kwa ajili ya kuboresha mchezo wa soka
Ali Bin al Hussein mwanamfale wa Jordan alijiondoa kabla ya kupigwa kura ya mkondo wa pili.
Blatter alikuwa akiungwa mkono na mashirikisho ya soka ya afrika Asia na Marekani Kusini huku Ali Bin al Hussein mwanamfale wa Jordanakiungwa mkono na UEFA.
Wakati huohuo,wafadhili wakuu wa shiriko la kandanda duniani FIFA wanasema kuwa wanatarajia raisi wake aliyechaguliwa kwa mara nyingine Sepp Blatter kuchukua hatua madhubuti ili kurejesha hadhi ya shirikisho hilo iliyochafuka.
Kampuni za Coca-Cola na McDonalds zimeitaka FIFA kuchukua hatua za haraka kwa munufaa ya mchezo wa soka na mashabiki kote duniani.
 Blatter alichaguliwa tena kwa muhula wa tano siku ya Ijumaa licha ya kuwepo uchunguzi unaofanywa na Marekani na Uswisi kuhusu kashfa zinazolikumba shirikisho hilo za ufisadi na ulaji rushwa dhidi ya maafisa wake wakuu.