Thursday, May 21, 2015

STERLING APATA MTETEZI

Liverpool:Sterling apata mtetezi

Nyota wa Liverpool Raheem Sterling ametetewa kwa kuwa na hamu kujiunga na vilabu vikubwa.
Mshambuliaji huyo wa Liverpool huenda asilaumiwe kwa kuonyesha hamu ya kung'aa zaidi na kutaka kushinda vikombe.
Hii ni kwa mujibu wa mshambuliaji wa zamani wa Blackburn,Chris Sutton.
Sterling mwenye umri wa miaka 20, anatarajia kumwambia meneja wa Liverpool Brendan Rodgers na mkurugenzi wa club hiyo Ian Ayre kuwa anataka kuihama Liverpool.
Tangu alipoanza kuonyesha nia yake yeye na wakala wake waliandamwa na kupingwa na wacheazaji wa zamani wa Liverpool.
"Sidhani kwamba uamuzi wake unahusu fedha" alisema Sutton
''Nahisi Sterling "anachotaka tu ni kujiunga na timu kubwa".
Sutton aliihama Blackburn na kujiunga na Chelsea kwa pauni milioni 10 mwaka 1999.

No comments:

Post a Comment