Wednesday, May 27, 2015

MIKOROGO YAINGIA BUNGENI

Haya ndio majina ya ‘mikorogo’ ambayo nimeijua leo baada ya Wabunge kuitaja Bungeni !!

2
Basi kama hukupata nafasi kuwa karibu na TV au radio yako kufuatilia Bunge la leo MAY 28 2015 Dodoma, kwenye maswali na majibu likawepo na hili linalohusu mkologo.. sikujua kabisa kwamba kumbe hii mikorogo ya urembo ina majina kabisa mtu wangu !!
Swali la kwanza lilihusu Serikali imejipangaje kuzuia mikorogo iliyopewa jina la king’amuzi na mchiriku?
Jibu: “TFDA imeandaa orodha yote ya vipodozi ambavyo havifai kwa matumizi ya binadamu, wananchi wanatakiwa wasitumie vipodozi hivyo kwa kuwa vina madhara.. mchiriku na ving’amuzi ni baadhi ya vipodozi visivyofaa kwa binadamu ”>> Juma Nkamia.
Baada ya jibu hilo wakasimama Wabunge wenye maswali mengine hapahapa kwenye mikorogo: “Dini zinakataza mwanadamu kujibadilisha, inavyoonekana Watanzania hatujaridhika Mungu alivyotujaalia… Nikimwambia Waziri tutoke tuingine barabarani atavikuta vipodozi visivyo na kiwango… Waziri anasemaje ili kuhakikisha wanawake na wanaume anawanusuru matatizo haya?”>>> Mbunge   Riziki Omar Juma.
Jibu: “Suala la kuiga limekuwa kubwa sana, tunapoiga tuige mambo mazuri… TFDA inafanya juhudi kukabiliana na vipodozi vinavyoingia nchini na havikidhi kiwango.. vingi vimekuwa vikiteketezwa”>>> Juma Nkamia.
Likaja swali jingine: “Viongozi wanatakiwa wame mfano ili raia wasifuate mtindo huu, Waziri anatuambia nini ili suala hili lianzie na Wabunge wenzetu wanaojipodoa na kuvaa nywele za bandia katika Bunge hili ili wawe mfano?” >>> Ibrahim Sanya.
Hili swali Naibu Spika Job Ndugai ikabidi alimalize juu kwa juu: “Hili swali sitaruhusu majibu, ni swali la uchokozi kwa Wabunge

No comments:

Post a Comment