Saturday, May 23, 2015

VIJANA WATAKIWA KUIGA MAZURI KUTOKA KWA MOPEROO INVESTMENT (BODABODA)


Tangakumekuchablog

Tanga, DIWANI viti maalumu (CCM)  kata ya Chumbageni Tanga, Saida Gaddaf, amewataka vijana kuunda vikundi vya Ujasiriamali ili kuweza kupata fursa za mikopo pamoja na asilima tano ya halmashauri ya jiji iliyotengwa kwa vijana.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya pikipiki 15 zilizotolewa na kampuni ya Fecon kwa Umoja wa madereva wa pikipiki na bajaj (Moperoo Investment) jana Gaddaf, aliwataka vijana kuunda vikundi kuchangamkia fursa za  mikopo.

Aliwataka vijana kuacha kubweteka wakati fursa ziko nyingi za kujiletea maendeleo na kuweza kupata asilimia tano zilizotengwa na halmashauri kwa ajili ya vijana.

“Najisikia fahari kuona vijana mumeunda umoja  ambao ni mfano wa kuigwa na kuweza kuaminiwa kwa kupewa pikipiki----hii ni fahari kwa wakazi wa kata yangu  na ni fahari kwa wakazi wa Tanga” alisema Gaddaf na kuongeza

“Kupitia hafla hii fupi ya makabidhiano niwambie vijana kuchangamkia fursa za mikopo kwenye taasisi za fedha pamoja na asilimia tano iliyotengwa kwa ajili ya vijana” alisema

Diwani huyo alitoa wito kwa vijana kuacha kujikalia vijiweni na kupiga soga jambo ambalo linaweza kuzalisha matukio mabaya yakiwemo ya uporaji na uvutaji wa bangi na hivyo Taifa kupoteza nguvu kazi.

Kwa upande wake, Afisa masoko kampuni ya Pikipiki (Fecon) ,Zakayo Liang, ameutaka umoja huo kuweka sheria nafuu za vijana ambao wanataka kujiunga  ili kuweza kupata fursa za kujikwamua na maisha.

Alisema kuwepo kwa sheria nafuu kutawawezesha vijana wengi kujiunga na vikundi vya ujasiriamali na kuweza kujikwamua na maisha jambo amblo litawawezesha pia kuepukana na magenge ya kihuni.

“Niweze kuwashauri ndani ya umoja wenu kuweka sheria nafuu zitakazomvutia kijana kujiunga----hii itapelekea kuondosha wimbi la vijana wasio na kazi” aliema Liang

Aliwataka kudumisha umoja na mshikamano ili kuweza kuwa chachu ya maendeleo na mfano kwa wengine ikiwa na lengo la kumkomboa kijana kutoka katika umasikini.

                                           Mwisho




Diwani kata ya Chumbageni Tanga , Telesphory Chambo (CCM) akipokea pikipiki 15 kutoka kwa Afisa masoko kampuni ya pikipiki aina ya Fecon, Zakayo Liang  zilizotolewa kwa Umoja wa Madereva wa pikipiki na bajaj (Moperoo Investment) zikiwa na lengo la kukopeshana ili kujikwamua na umasikini. Kushoto ni Diwani viti maalumu kata ya Chumbageni, Saida Gaddaf (CCM)  na katikati ni Mwenyekiti wa Moperoo, Silas Stivin.






 Afisa Masoko kampuni ya pikipiki (Fecon), Zakayo Liang (kulia) akimkabidhi pikipiki 15, Afisa Maendeleo ya Vijana, Enersest Shekibua kwa niaba ya Umoja wa madereva wa pikipiki na bajaj (Moperoo Investment) ya mjini Tanga na makabidhiano kufanyika katika viwanja vya umoja huo jana.

Afisa masoko kampuni ya utengenezaji pikipiki aina ya Fecon , Zakayo Liang, akimkabidhi funguo za pikipiki 15 Diwani viti maalumu kata ya Chumbageni  , Said Gaddaf  (CCM), zikiwa ni kuwasaidia vijana kujiajiri na kujikwamua kiuchumi makabidhiabno yaliyofanyika jana viwanja vya umoja huo.

No comments:

Post a Comment