Friday, May 22, 2015

IRELAND KUPIGA KURA KUHALALISHA AU KUKATAA NDOA YA JINSIA MOJA

Ishu ya ndoa za jinsia moja imechukua headlines tena, Ireland wameamua kupiga kura leo !!

IRELAND-master675Mwaka 1993 nchi ya Ireland ilikuwa moja ya mwisho mwisho kabisa katika nchi za Ulaya kuhalalisha ishu ya uhusiano wa jinsia moja.. mpaka leo ni miaka 22 imepita, wakati wowote huenda kukatokea headline nyingine kuhusu suala hilo, Bunge liliamua hii ishu washirikishwe watu wao pia na mpaka kesho Jumamosi May 23 2015 tutasikia nini kimepitishwa.
Watu wa Ireland wanaendelea kupiga kura leo, kama kura nyingi zikisema YES, basi Katiba ya nchi hiyo itafanyiwa mabadiliko na ishu ya ndoa za watu wenye uhusiano wa jinsia moja zitakuwa zimeruhusiwa rasmi kwenye nchi hiyo !!
Kuna vitu vingi vinaendelea Ulaya, Marekani na nchi nyingine ikiwemo hii ya kuhalalisha ndoa na uhusiano wa jinsia moja, kwa Afrika ni nchi chache zimetoa msimamo.. Uganda ni moja ya nchi ambazo zilikataa kuhalalisha ndoa za aina hiyo.
Ireland VITEKampeni zimeendelea mtaani, migahawani kuna mabango yaliyoandikwa “YES EQUALITY” kuonesha watu kwamba wapo watu ambao wako tayari kuyakubali mabadiliko hayo.
IRELAND-master675Usiwe mbali nami kila peruz kwa kupata habari matukio na michezo , ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment