Wednesday, May 27, 2015

ADONDOKA BAHARINI BAADA YA JARIBIO LA KUPIGA PICHA YA SELFIE

Mwanafunzi alitaka Selfie ya kipekee juu ya Mlima…kilichofuata ni Story!!

selfie
Matumizi ya picha za Selfie sasa yameanza kuleta madhara kwa baadhi ya watu ambao hutamani kupiga picha za kipekee za aina hiyo.
Pamoja na upigaji wa picha hizo kuzidi kuongeza umaarufu katika maeneo mengi duniani lakini kuna stori nyingi ambazo zimekua zikitokea zinazohusu watu kupoteza maisha kutokana na jinsi wanavyopiga picha hizo.
Tangakumekuchablog iliwahi kuandika stori ya binti mmoja kupoteza maisha baada ya kutamani kupiga picha ya selfie ya kipekee ambapo alipanda juu ya treni iliyokua ikitembea ili tu aweze kupata picha hiyo na badala yake alipoteza maisha baada ya kupigwa na shoti ya umeme huku wenzake wakijeruhiwa vibaya.
Leo tena kumetoka Stori inayofanana na hiyo baada ya mwanafunzi mmoja wa chuo huko Indonesia kupoteza maisha baada ya kujaribu kupiga picha ya selfie kwenye ukingo wa mlima ambao kwa chini kulikuwa na bahari.
Mohamed Aslam ambaye ni raia wa Singapore alifikwa na mauti baada ya kudondoka baharini ikiwa ni urefu wa futi sita wakati akichukua picha hiyo katika visiwa vya Lembongan.
Baadhi ya mashuhuda ambao walikua marafiki zake walisema mwanafunzi huyo alikufa baada ya kutokea upepo mkali uliomdondosha na baadaye mwili wake ulipatikana pembezoni mwa bahari hiyo na alipofikishwa hospitali tayari alikua amefariki.
Kwa habari na matukio kedekede ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment