Wednesday, May 27, 2015

KIWANDA CHA SARUJI TANGA CHATOA MIFUKO 300 UJENZI WA KITUO CHA AFYA KISIMATUI TANGA



Tangakumekuchablog

Tanga,KIWANDA cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga, kimetoa mifuko 300 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya  kijiji cha Kisimatui ili kuondosha kero ya kufuata matibabu masafa marefu kwa wakazi wa eneo hilo na vijiji vya jirani.

Akizungumza wakati wa halfa fupi ya makabidhiano juzi, Meneja Biashara kiwanda cha Saruji cha Simba Cement, Mattheus Roos, alisema msaada huo umekuja baada ya maombi ya wakazi wa kijiji cha Kisimatui na maeneo jirani kwa muda mferu wamekuwa wakifuata matibabu masafa marefu.

Alisema kufuatia kero hiyo kiwanda cha saruiji kiliguswa na kuona ili kuweza kupatikana kito cha afya ni vyema kutoa mifuko 300 ya saruji na kuikabidhi kwa viongozi wa kijiji kwa kuanza ufyatuaji wa matofali.

“Kiwanda cha saruji imetoa mifuko mia tatu yenye thamani zaidi shilingi milioni tatu na laki tano-----ni sera ya kiwanda kusaidia jamii ikiwemo elimu na mazingira” alisema Roos na kuongeza

“Kiwanda itahakikisha kituo kinajengwa haraka na kukamilika kama ilivyopangwa na tutakuwa bega kwa bega na wananchi -----ni imani yetu kituo hiki kitakuwa msaada pia kwa vijiji vya jirani” alisema 

Kwa upande wake diwani kata ya Pongwe (CCM), Uzia Juma, alisema msaada huo utatumika kama ulivyopangwa na kuyataka makampuni mengine kuiga ili kuweza kukamilisha ujenzi wa kituo cha afya.

Alisema kwa muda mrefu wakazi wa vijiji vya Kisimatui, Pongwe na Kichangani wamekuwa katika wakati mgumu wa kupata matibabu na badala yake wamekuwa wakisafiri masafa marefu.

“Kwa miaka mingi wakazi wa Kisimatui na vijiji vya jirani wamekuwa wakifuata matibabu umbali zaidi ya kilometa kumi---- ujio wa kituo hiki itakuwa mkombozi kwa wengi na asanteni kiwanda cha saruji” alisema Juma

Aliwataka wananchi na viongozi wa kijiji cha Kisimatui kushirikiana  kuwezesha kujengwa kwa kituo hicho na kutaka kutumiliwa kwa saruji hiyo kama ilivyopangwa.

                                                   Mwisho

No comments:

Post a Comment