Wednesday, May 27, 2015

FIFA NDANI YA TUHUMA NZITO

FIFA kwenye tuhuma za rushwa, kuna hawa maafisa wana kesi ya kujibu…

sep
Wakati uchaguzi mkuu wa Shirikisho la soka dunia FIFA ukitarajiwa kufanyika keshokutwa, leo kuna taarifa mpya kutoka ndani ya shirikisho hilo.
Kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa mashabiki wa soka duniani ambao wamekuwa wakilalamikia utendaji mbovu wa viongozi walioko madarakani na hadi kupelekea wagombea waliokuwa wakiwania nafasi ya Urais ndani ya Shirikisho hilo kuamua kujindoa.
webb
Makamu wa Rais wa FIFA Jeffrey Webb
Taarifa mpya zinadai kukamatwa kwa tuhuma za rushwa kwa maafisa sita wa Shirikisho hilo wakiwa katika hoteli moja ya kifahari mjini Zurich, Switzerland.
Maafisa hao ni pamoja na makamu wa Rais wa FIFA, Jeffrey Webb na wanashikiliwa wakisubiri kupelekwa Marekani kwa ajili ya uchunguzi huku Rais Blatter naye akiwa mmoja wa washtakiwa wlaiokuwa wakichunguzwa kwa muda mrefu lakini hayupo kwenye orodha ya waliokamatwa.
Shutuma hizo zinahusisha rushwa ya kiasi cha dola milioni 150 kwa kipindi cha miaka 20 ambazo zilikuwa zikichunguzwa na wapepelezi kutoka Marekani.
Wanachama wa Fifa watakutana mjini Zurich kwa ajili ya mkutano wao wa mwaka siku ya ijumaa wakati rais wa Shirikisho hilo Sepp Blatter akiwa anawania nafasi hiyo kwa muhula wa tano akiwa amebaki peke yake.
Kwa matukio na habari usiwe mbali nami ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment