Monday, May 25, 2015

JAMII YATAKIWA KUWA NA ADA YA KUJUA AFYA ZAO

Tangakumekuchablog

Tanga,JAMII imetakiwa kuwa na ada ya kupima afya zao ili  kuweza kujitambua na kutakiwa  kuacha kuficha magonjwa jambo ambalo linaweza  kupunguza nguvu kazi ya Taifa.

Akizungumza wakati wa upimaji afya na uchangiaji damu salama zoezi lililoendeshwa na Mfuko wa Afya jamii (NSSF), Mratibu wa Udhibiti wa magonjwa ya Ukimwi Tanga, Suleiman Hassan, alisema watu wengi hawana ada ya kupima afya zao.

Alisema hali hiyo imekuwa ikichangia kushuka kwa kiwango cha uzalishaji mali baada ya watu wengi kuugua majumbani na kuogopa kupima afya zao katika vituo vya afya.

“Tuseme ukweli kuwa hatuna ada ya kujua afya zatu na badala yake tunapoteza nguvu kazi kwa kuugulia maradhi ndani ya miili yetu----hebu tuthubutu jamni kutambua afya zetu sio dhambi” alisema Hassan

“Utamkuta mtu anaugua malaria au magonjwa ya tumbo wakati hospitali zimemzunguka hata ile kusema japo kipimo kimoja ngoja niendele mtu hataki anataka kufa na tai shingoni” alisema

Aliitaka jamii kubadilika kwa kuwa na ada ya kuhudhuria vituo vya afya kwa kupima ili kutambua magonjwa mtu yanayomsibu na kuacha kuugulia maradhi kitandani jambo ambalo linaweza mtu kukaribisha mauti.

Kwa upande wake, Meneja wa Bima ya Afya Tanga, Ali Mtulya, amesema watu wengi wanaopata magonjwa ya shinikizo la damu na presha ni kutokana na kutofanya mazoezi na kula vyakula bila mpangilio.

Alisema kula bila npangilio na kuacha kufanya mazoezi kunamfanya mtu kupata magonjwa na hivyo kuwataka kuwa na ada ya kupima afya zao na kufuata  maelekezo ya wataalamu wa tiba.

“Watu wengi wanaacha kufanya mazoezi ya kujenga mwili na kusahau kuwa ni moja ya kuimarisha afya  kuepuka magonjwa yakiwemo presha na mafuta mwilini----tubadilikeni ulimwengu huu ulioacha vyakula vya asili” alisema Mtulya

Aliitaka jamii kujipenda kwa kufanya mazoezi na kupima afya zao kila baada ya muda jambo ambalo litaifanya miili yao kuwa imara na kuepuka magonjwa ya mara kwa mara.
                                                        Mwisho

No comments:

Post a Comment