Monday, May 25, 2015

JOTO KALI LAUWA WATU 500 INDIA

India kwenye Headlines..Idadi ya vifo vya watu vilivyotokana na joto kali

INDIA4
Moja ya nchi zenye kiasi kikubwa cha joto duniani ni pamoja na India ambayo unaambiwa kwa sasa joto lake linafikia nyuzi joto 48 katika maeneo mengi.
indiA2
Taarifa ambayo si nzuri kutoka nchini humo zinasema watu wapatao 500 wamepoteza maisha kufuatia kuongezeka kwa joto huku idara ya utabiri wa hali ya hewa ikisema hali hiyo ya juu ya joto inatokana na kukosekana kwa mvua kwa muda mrefu.
Maafisa utawala wameanza kampeni ya kuwahamasisha wananchi kukaa majumbani mwao na kuwashauri wanywe waji mengi.
INDIA3
Majimbo yaliyoathirika ni pamoja na Andra Pradesh ambalo ndilo lililoongoza kwa kupoteza idadi kubwa ya watu waliofikia 246.
Vifo vingi zaidi vimeripotiwa katika majimbo ya kusini ya Telangana na Andhra Pradesh, ambapo watu 140 wamepoteza maisha yao kuanzia siku ya jumamosi hadi leo wakati wimbi hilo la joto lilipotokea.
india
Mji wa Allahabad ulioko Uttar Pradesh ulisajili vipimo vya nyuzi joto 48C huku wakazi wa mji mkuu wa India, New Delhi ukiwa na kiwango cha nyuzijoto 44C .

No comments:

Post a Comment