Saturday, July 30, 2016

ASILIMIA 50 YA WATOTO WANA MAGONJWA YA MENO

50% ya watoto Tanzania wana magonjwa ya meno - TDA

Chama cha Madaktari wa Kinywa na Meno Tanzania (TDA), wakati kikiadhimisha Siku ya Afya ya Kinywa na Meno Duniani mwaka huu kilibaini kuwa zaidi ya asilimia 50 ya watoto walio chini ya miaka 14, wanakabiliwa na magonjwa ya kinywa na meno.

Pia kiilibaini kuwa asilimia 80 ya watanzania wanakabiliwa na matatizo ya ugonjwa wa fizi.

Katika kukabiliana na hali hiyo, wadau mbalimbali wameanza kutoa elimu ya afya ya kinywa ikiwa ni pamoja na watengenezaji wa dawa ya meno ya whitedent wa namna ya kujikinga na magonjwa ya kinywa.

Wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliozungumza na East Africa Radio wanasema kumekuwa na upuuziaji mkubwa katika usafishaji wa meno, ulimi na kinywa kwa ujumla hali inayochangia watu wengi kung'oa meno yao.

No comments:

Post a Comment