Friday, July 29, 2016

UFARANSA KUPIGA UFADHILI WA NJE WA MISIKITI

Ufaransa kupinga ufadhili wa nje wa misikiti

Waziri mkuu wa Ufaransa Manuel Valls amesema kuwa huenda akapendekeza kupigwa marufuku kwa muda ufadhili wa misikiti kutoka nje kufuatia mashambulio ya hivi karibuni yanayotekelezwa na wana jihad.
Akizungumza na gazeti la Le Monde ,bwana Valls pia amewataka maimamu wote wa Ufaransa kupewa mafunzo ndani ya Ufaransa na wala sio nje ya taifa hilo.
Amesema ni wakati ambapo Ufaransa inafaa kujenga uhusiano mpya na Islam,akitaja vita dhidi ya itikadi kali kama jukumu la kizazi hiki.
Serikali ya Ufaransa imekosolewa kwa kushindwa kuzuia mashambulizi matatu katika kipindi cha miezi 18 iliopita.

No comments:

Post a Comment