Wednesday, July 27, 2016

CLINTON AMPIGIA CHAPUO HILLARY

Bill Clinton: "Rafiki yangu" Hillary anafaa kuwa rais

Clinton
ClintonRais wa zamani wa Marekani Bill Clinton amemsifu sana mkewe Hillary na kusema anafaa kuongoza taifa hilo.
Ameambia kongamano kuu la chama cha Democratic mjini Philadelphia kwamba mkewe ndiye “mfumaji bora zaidi niliyewahi kukutana naye”.
Kwenye hotuba yenye hisia kali, amemweleza Hillary kama “rafiki mkubwa” na akasimulia walivyokutana na jinsi anavyojitolea katika utumishi wa umma.
Saa chache awali, mkewe aliibuka kuwa mwanamke wa kwanza nchini Marekani kuidhinishwa kuwania urais na chama kikubwa
Bi Clinton alihitimisha shughuli za usiku huo wa Jumanne kwa ujumbe wa video.

No comments:

Post a Comment