Tuesday, July 26, 2016

JAMAA ANAEWATOA USICHANA WASICHANA ATIWA MBARONI

jamaa anayewatoa mabinti wa kike usichana Malawi imeifikia Serikali

Raia mmoja wa Malawi alionekana katika habari moja ya BBC akihusishwa na tambiko la usafishaji wa wasichana wadogo kupitia kushiriki ngono nao amekamatwa.
Eric Aniva amekamatwa kufuatia agizo la Rais Peter Mutharika kulingana na mkurugenzi wa mawasiliano ikulu ya Rais, Bright Molande aliyezungumza na BBC, Molande amesema kuwa  kutokana na uovu huo Aniva atashtakiwa kwa kukiuka haki za watoto.
Aidha aliongeza kuwa Rais amechukizwa na yaliofichuliwa katika habari hiyo na ameapa kukabiliana na tamaduni hiyo. Mtu aliyetajwa katika habari hiyo ambaye alifanya mapenzi na zaidi ya wasichana 100 pia imebainika kuwa alikuwa na virusi vya ugonjwa wa UKIMWI.
Source; BBC

No comments:

Post a Comment