Wednesday, July 20, 2016

WATOTO WA TRUMP WANOGESHA KONGAMANO LA REPUPLICAN

Wanawe Trump wafana kongamano la Republican

Trump JuniorWana wawili wa mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump ni miongoni mwa watu waliohutubu katika kongamano la kitaifa la chama hicho mjini Cleveland, Ohio.
Kinyume na mkewe Trump, Melania, ambaye alishutumiwa sana alipotoa hotuba siku ya kwanza baada ya kubainika kwamba baadhi ya maneno kwenye hotuba yake yalitoka kwenye hotuba iliyotolewa na mke wa Rais Barack Obama, Michelle, mwaka 2008, wawili hao walisifiwa sana.
Mwanawe wa kiume, ndiye aliyetangaza kwamba babake alikuwa amepata wajumbe wa kutosha na kuidhinishwa kuwa mgombea rasmi wa chama hicho.

No comments:

Post a Comment