Sunday, July 31, 2016

MAFURIKO YAUWA WATU 100 INDIA

Mafuriko yaua zaidi ya watu 100 India na Nepal

Mafuriko mashariki mwa India na nchini Nepal yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 100 na kuwaathiri mamilioni ya wengine.
Mito iliyojaa maji imesababisha vijiji kufurika na kuwalazimu maelfu ya watu kuhama makwao.
Katika majimbo ya India ya Assam na Bihar, makundi ya uokoaji yanatumia mashua kuwafikia watu ambao wametafuta hifadhi katika makao ya muda kwenye sehemu zilizoinuka.
BBC

No comments:

Post a Comment