Saturday, July 30, 2016

FAIBER YA KISASA YATENGENEZWA TANGA, ITAKUWA NA UWEZO WA KUBEBA ABIRIA 80

 Mafundi wakiunda Faiber ambayo kukamilika kwake itakuwa na uwezo wa kuchukua abiria zaidi ya 80 waliokaa na kuondosha kero ya Usafiri kati ya Pemba na Tanga.
Faiber hiyo ambayo itakuwa ya kwanza kutengenezwa Tanzania hususani Tanga tofauti na ilivyo huwa inaagiziwa kutoka nje ya nchi.
Faiber hiyo inayotengezwa na Mtaalamu, Hemed Said mkazi wa Kojani Pemba.
Inatajwa kuwa Faiber hiyo ambayo kukamilika kwake itakuwa msaada mbali ya kubeba abiria pia inaweza kufanya uokozi kutokana na kuwa na Spidi kubwa  kufika kwenye tukio.





Hii ndio Faiber ambayo kukamilika kwake itakuwa na uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 80 na kuwa na uwezo wa kutembea kwa kasi zaidi ya vyombo vyengine baharini

No comments:

Post a Comment