Sunday, July 31, 2016

CHALSEA KUVUNJA KABATI KUMNUNUA LUKAKU

Chelsea sasa wapo radhi kutoa zaidi ya Tsh Bilioni 190 kwa ajili ya Lukaku

Dirisha la usajili la msimu huu kwa vilabu vya soka barani Ulaya linazidi kuvutia zaidi, hii inatokana na vilabu vingi sasa kutaka kuwarudisha katika timu zao wachezaji wao wa zamani kwa gharama kubwa wakati waliwaacha waondoke kirahisi misimu kadhaa iliyopita.
Man United wanataka kuvunja rekodi ya usajili kwa kumridisha Pogba, Real Madrid wamemrudisha Morata kikosini, Borussia Dortmund tayari wamemrudisha Mario katika kikosi chao, sasa Chelsea inajiandaa kutoa euro milioni 80 kwa ajili ya kuishawish Everton imuachie mchezaji wao wa zamani Romelu Lukaku arejee Stamford Bridge.
Lukaku-Chelsea
Mwandishi Ivan Zazzaroni wa gazeti la dello Sport ameandika katika gazeti kuwa Chelsea wapo tayari kutoa euro milioni 80 kwa ajili ya kumrudisha mshambuliaji wao Romelu Lukaku aliyeondoka Stamford Bridge 2014, Lukaku ameondoka Chelsea akiwa kacheza mechi 10 katika kipindi cha miaka mitatu alipojiunga nayo akitokea Anderlecht.
millardayo

No comments:

Post a Comment