Friday, July 22, 2016

POGBA APEWA NAMBA 6 MAN UNITED

Man United yaweka hadharani namba za jezi za wachezaji wao, namba 6 ni ya Pogba

Timu ya Manchester United imeweka hadharani namba ya jezi za wachezaji wao watakazozitumia kwa msimu wa mwaka 2016/2017.

Mshambuliaji mpya aliyesajiliwa hivi karibuni kwa uhamisho huru, Zlatan Ibrahimovic amekabidhiwa jezi yenye namba aliyozoea kuvaa muda mrefu yenye namba 9 iliyokuwa ikivaliwa na Antonio Martial klabuni hapo na sasa mchezaji huyo atakuwa anavaa jezi yenye namba 11 iliyokuwa ikivaliwa na nguli wa timu hiyo Giggs na kinda Januzaj.

Aidha kwenye orodha iliyotolewa na timu hiyo inaonyesha kuwa jezi namba 6 haijapata mvaaji huku kukiwa na taarifa kuwa imewekwa maalumu kwa kiungo Paul Pogba anayetarajiwa kutua klabuni hapo kwa uhamisho utakaoweka rekodi ya dunia wa paundi milioni 100.


No comments:

Post a Comment