Saturday, July 23, 2016

WANAFUNZI 160 DARASA MOJA, SHULE YA MSINGI MKWAKWANI TANGA



Tangakumekuchablog
Tanga, SHULE ya Msingi Mkwakwani halmashauri ya jiji la Tanga, yenye wanafunzi 1,223 inakabiliwa na uhaba wa madawati na wanafunzi kulazimika kusomea chini.
Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Aidan Kassian  akizungumza na waandishi wa habari waliofika kutaka kujua  changamoto inayoikabili shule hiyo baada kuwa ya mchanganyiko na shule ya Bombo kufuatia majengo yake kuwa chakavu na wananfunzi  kulazimika kuhamia shuleni hapo.
Alisema kuna changamoto nyingi ikiwemo wingi wa wanafunzi kurundikana darasa  moja na wengine kulazimika kukaa chini kufuatia uhaba wa madawati na kuwa kero kwa wanafunzi.
“Shule yangu changamoto kubwa ni uhaba wa madawati na madarasa baada ya shule ya bombo kuhamia hapa kufuatia majengo yao kuwa hatarishi, madarasani kuna mrundikano wa wanafunzi” alisema Kassian na kuongeza
“Kwa wingi huu wa wanafunzi napatwa na kitisho cha kuzuka kwa magonjwa ya miripiko kwani tuko na matundu ya kumi na nne ambapo saba ni ya  wanaume na saba kwa wanawake” alisema
Alisema kuna baadhi ya madarasa wamekuwa wakilazimika kuwaweka wanafunzi 160 kwa darsa moja jambo ambalo limekuwa kero kubwa kwa mwalimu kufundisha na kumfikia mwanafunzi mmoja mmoja.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya shule, Sauda Singo, alisema zinahitajika jitihada za kuhakikisha changamoto za madawati na vyoo kupatiwa ufumbuzi wa mara moja ukiwemo wa uzio wa shule.
Alisema shule hiyo haina uzio jambo ambalo linawafanya wanafunzi kutoka na kuingia bila mpangilo na kushindwa kuwadhibiti na ulinzi wakati wa usiku.
“Shule haina uzio jambo linalowapelekea wanafunzi kuingia na kutoka bila mpangilio pamoja na kushindwa kuwatambua na kuwadhibiti “ alisema Singo
Alisema ili kuendana na kasi ya elimu amewaomba wadau wa elimu kutoa msaada kwa shule hiyo kipindi hiki cha mchanganyiko wa shule mbili kufuatia ya Bombo kuwa chakavu na kuhatarisha usalama wa wanafunzi darasani.
                                                 Mwisho



 Wanafunzi wa shule ya awali ya Mkwakwani halmashauri ya jiji la Tanga Tanga, wakiandika chini kufuatia uhaba wa madawati shuleni hapo. Darasa hilo liko na wanafunzi 161.




 Wanafunzi wa shule ya Msingi darsa la 4  Mkwakwani halmashauri ya jiji la Tanga, wakisomea chini kutokana na uhaba wa madawati shuleni hapo, shule ni mchanganyiko na shule ya msingi ya Darajani baada ya wanafunzi kuhamishwa kutokana na uchakavu. Darasa hilo liko na wanafunzi 163 ambao husoma kila siku.
Kwa habari, matukio na michezo ni hapahapa Tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment