UNDANI WA KIFO CHA KEPTENI JOHN KOMBA!
Marehemu Kapteni Komba.
HabariKwa hisani ya http://www.globalpublishers.info/
Picha ya kwanza ya Marehemu komba mara baada ya kufariki dunia.
…Komba enzi za uhai wake.
MBUNGE wa Mbinga Magharibi, Kapten John Komba amefariki dunia jioni hii jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amethibitisha kutokea kwa kifo hicho, hata hivyo hakuwa tayari kuelezea kwa undani kwa madai kuwa taarifa hizo zimemfikia sasa hivi.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amethibitisha kutokea kwa kifo hicho, hata hivyo hakuwa tayari kuelezea kwa undani kwa madai kuwa taarifa hizo zimemfikia sasa hivi.
Mmoja
 wa watoto wa Komba ambaye aliyejitambulisha kwa jina la Herman 
amethibitisha kutokea kwa msiba huo na akasema, huku akilia, msiba wa 
baba yake upo nyumbani kwake Mbezi Tangi Bovu, Dar.
Habari
 zinasema asubuhi ya leo Komba alikwenda kwenye shughuli zake za kikazi 
kama kawaida lakini baadaye akajisikia vibaya, hivyo akaamua kurudi 
nyumbani ambako alizidiwa ndipo familia yake ilipoamua kumkimbiza 
Hospitali ya TMJ lakini alipopimwa na madaktari ikathibitika kuwa 
alikuwa tayari ameaga dunia. habari zaidi zinasema kuwa hivi sasa mwili 
wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Jeshi ya Lugalo.
Kapteni
 Komba ambaye pia ni Mkurugugenzi wa Kikundi cha Maigizo cha Tanzania 
One Theatre (TOT),  ambacho kina kikundi cha taarabu na bendi  
inayokwenda na mtindo wa Achimenengule, amekuwa akikisaidia sana chama 
chake, Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kampeni zake wakati wa uchaguzi 
kwa kutunga nyimbo za kuhamasisha wapiga kura na kushiriki kupiga live 
kwenye majukwaa ya kisiasa.
…alipokuwa bungeni
Enzi
 za uhai wake alitamani  sana na kufanya juhudi kubwa ili mtindo wa 
Achimenengule uwe wa kitaifa lakini ikashindikana,  na badala yake 
Watanzania sasa tuna muziki wa Mduara ambao umekuwa kama mtindo wa 
muziki wetu kwa sababu zifuatazo.
Kwanza,
 ni mtindo halisi wa Kitanzania uliochipuka kutoka mahadhi ya kimwambao 
ya Tanzania. Pili, ndiyo mtindo pekee uliowahi kutumiwa na bendi nyingi 
baada ya kuasisiwa na ‘mabingwa’ wa muziki wetu, wana Njenje, The 
Kilimanjaro Band.
Baada
 ya bendi hiyo kuuasisi, mtindo huo, tayari umepigwa na bendi kama TOT 
Plus, Chuchu Sound, Pamo Sound, Inafrika Band, wana mipasho kadhaa na 
mwanamuziki mahiri lakini asiyethamini kiwango chake kikubwa cha muziki,
 Bob Haisa.
Sababu
 ya tatu ni kwamba mtindo huo umekuwa wa kupigwa na bendi nyingi, 
vikundi vingi na wanamuziki wengi si kwa kulazimisha bali kwa mapenzi tu
 ya mashabiki wa muziki wa Tanzania.
Kapteni
 Komba awali alikuwa mwalimu wa shule ya msingi kabla ya kuingia jeshini
 na kuwa kiongozi wa kikundi cha maonesho cha jeshi na baadaye Rais 
Mstaafu Ali Hassan Mwinyi akamshawishi aachane na jeshi na kujiunga na 
CCM wakati wa mfumo wa vyama mingi ulipoingizwa mwaka 1992.
“Mzee
 Mwinyi ndiye aliyenifanya niache jeshi wakati huo nikiwa na cheo cha 
ukapteni. Aliniomba nikisaidie chama kwa kuanzisha kikundi ambacho lengo
 lake lilikuwa kukipigia debe CCM,” aliwahi kusema hivyo Kapteni Komba.
Ameshiriki
 kampenzi za marais Ally Hassan Mwinyi, Benjamin William Mkapa na aliye 
madarakani hivi sasa, Jakaya Mrisho Kikwete. Alikuwa Mjumbe wa 
Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi hadi
 kifo kinamchukua.
Licha ya siasa Kapteni Komba alikuwa anamiliki shule na pia alikuwa na biashara kadhaa.
Mwaka 2012 Komba aliwahi kupelekwa India kwa matibabu ambapo alifanyiwa upasuaji wa nyonga baada ya kupata ugonjwa uliosababisha mifupa kusagana sehemu hiyo ya nyonga.
Mwaka 2012 Komba aliwahi kupelekwa India kwa matibabu ambapo alifanyiwa upasuaji wa nyonga baada ya kupata ugonjwa uliosababisha mifupa kusagana sehemu hiyo ya nyonga.
Baada
 ya kurejea nchini alisema upasuaji huo ulichukua saa tano na ulifanyika
 katika Hospitali ya Apollo, India na alikanusha kuwa alikuwa na ugonjwa
 wa figo.Ugonjwa uliomuua ni shinikizo la damu ambalo lilikuwa 
likimsumbua kwa muda mrefu.
..marehemu
 Komba akiongea na wanahabari nyumbani kwake Mbezi tangi Bovu akielezea 
kuimarika kwa afya yake aliporejea kutoka India kwenye matibabu, Julai 
27, 2012.
Marehemu Komba ameacha mjane, 
Bi Salome, ambaye ni mwalimu kitaalumu na watoto kadhaa. Mungu ailaze 
roho ya marehemu mahali pema peponi- ameen!




 




















 Kama kawaida tangakumekuchablog inakuletea kurasa za mwanzo mwisho za magazeti kila siku kupitia www.tangakumekuchablogspot.com
Kama kawaida tangakumekuchablog inakuletea kurasa za mwanzo mwisho za magazeti kila siku kupitia www.tangakumekuchablogspot.com




