Saturday, February 28, 2015

KAULI YA MWISHO YA JOHN KOMBA

Alichofanya Kapteni Komba kwa familia yake siku mbili kabla ya kifo chake.

capt KombaKifo cha Mbunge wa Mbinga Magharibi na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya taifa CCM kapteni John Komba ambaye amefariki dunia akiwa hospital ya TMJ jana 28 kilitanguliwa na kitu ambacho kinadhaniwa kama kilikua ni ishara ya siku yake ya mwisho.
Claudia John Komba ambaye ni mtoto wa 9 kati ya watoto 11 wa marehemu John Komba amesema nna kuelezea baadhi ya vitu ambavyo kwao imekua kama kauli ya mwisho kutoka kwa Baba yao ambayo aliitoa siku ya sherehe ya kuzaliwa kwake.
Claudia ‘Taarifa ilinifikia mida ya saa 9 akasema anajisikia vibaya ambapo wakati yupo njiani akawa anaweweseka sana, tulipofika TMJ hospital walipofanya vipimo walisema ameshafariki’
Claudia John Komba: ‘Zilikuwepo baba alikua amekaa ilikua mida ya asubuhi akawa analalamika anajisikia vibaya tukampeleka hospitali, tukagundua sukari imepanda sana na presha imepanda sana, akatolewa akawa anaendelea vizuri’
‘Juzi tarehe 26 february ilikua siku yangu ya kuzaliwa, akaita watoto wote akasema nataka kufanya birthday sababu birthday nyingi huwa zinanipita nakua nipo nje, akatukusanya watoto wote, aliongea maneno ya mwisho akatusihi watoto tupendane tusiweke  matabaka kwamba huyu mdogo huyu mkubwa alisema yeye hana mkataba na Mungu’.

No comments:

Post a Comment