Saturday, February 21, 2015

MSIMAMO WA LIGI KUU ENGLAND

Nimekuwekea hapa msimamo wa ligi na matokeo ya Chelsea vs Burnley

(null)
Ama kwa hakika leo haikuwa siku nzuri kwa vijana wa Jose Mourinho – klabu ya Chelsea.
Wakicheza dhidi ya moja ya timu zinazopigania kutoshuka daraja – Burnley, Chelsea leo imempoteza mchezaji wake muhimu Nemanja Matic ambaye amefungiwa mechi 3 kutokana na kupata kadi nyekundu ya moja kwa moja.
Wakiwa kwenyee uwanja wao wa nyumbani – Stamford Bridge, Chelsea walipunguzwa kasi baada ta kutoka sare ya 1-1 na Burnley.
Chelsea walianza kupata goli mapema katika dakika ya 16 ya mchezo huo mfungaji akiwa Branslav Ivanovic, lakini huku baadhi ya mashabiki wakijua leo Chelsea wangetoka na ushindi – Burnley wakasawazisha kupitia goli la Ben Mee katika dakika za mwisho za mchezo huo.
Kwa matokeo hayo Chelsea wanaendelea kushika usukani mwa EPL huku wakifukuziwa na City.
(null)

No comments:

Post a Comment