Wednesday, February 25, 2015

WAZAZI WAKERWA NA TABIA ZA BINTI YAO

Wazazi hawakupendezwa na uhusiano wa mtoto wao na boyfriend wake, wakaamua hivi..

girl
Siku za nyuma kulikuwa na story ambazo tuliwahi kuzisikia ama watu wazima wanaweza kukumbuka enzi hizo wazazi wanakuchambulia mchumba au mpenzi wa kuoa ama kuolewa, hii siku hizi inaonekana kuwa imepungua kwa kiasi kikubwa, kumbe sio sisi peke yetu wenye tuliowahi kuwa na utamaduni huu.
Story inatoka China, msichana Zhang Qi ambaye ana miaka 24 amekuwa akiishi kwa kunyanyaswa na familia yake tangu mwaka 2009 ambapo alifungiwa ndani ya chumba na wazazi wake ambao waliamua hivyo kutokana na kutopendezwa na mtoto wao kuwa na uhusiano na kijana wa kiume ambaye wao hawakupendezwa naye.
PAY-Zhang-Qi
Hii ndio nyumba aliyofungiwa msichana huyo kwa miaka sita.
Wazazi walifanya maamuzi hayo magumu kama njia ya kuwatenganisha huku wakiwadanganya majirani kwamba msichana huyo ana matatizo ya akili ndio  maana wameamua kumfungia ndani muda wote na kumhudumia kila kitu ndani ya chumba kwa muda wote huo.
PAY-Zhang-Qi (1)habgf
Picha zikionesha nje na ndani ya chumba alichofungiwa Zhang
Majirani wanasema wazazi wake ni wakali na hawakutaka jirani yoyote kujihusisha na ishu ya msichana huyo hivyo ikawa ngumu kujua kama ni kweli ana matatizo ya akili au hapana.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumecha.com

No comments:

Post a Comment