Monday, February 23, 2015

JAY Z NA BEYONCE WAPANGISHA NYUMBA LOS ANGLES

Jay Z na Beyonce ndani ya mjengo huu wa kupanga tena, wamekosa nyumba ya kununua

bey2Kabla ya kufanya maamuzi haya Beyonce na Jay Z walikaa zao hotelini, hiyo ilikuwa baada ya kutafuta nyumba ya kuishi kwa muda mrefu bila kupata.
Maamuzi yao kwa sasa ni kurudi kwenye hii nyumba ya kupanga ndani ya Los Angeles, Marekani ambayo waliwahi kuishi mwaka jana pia, hii inakuja baada ya kukosa nyumba ambayo itaendana na hadhi yao, ishu nyingine ambayo ningependa na wewe uifahamu ni kiasi cha pesa ambacho mastaa hao watakuwa wakilipia kodi kwenye nyumba hiyo waliyopanga, pesa hiyo ni dola laki moja na nusu (USD 150,000/-) ambayo kwa hela yetu ni kama milioni 270/-, lakini mwaka jana walikuwa wakilipia dola laki 2.
Hapa kuna PICHAZ za nyumba hiyo ambayo mastaa hao wanarudi kwa mara ya pili kuendelea na maisha yao ndani ya Los Angeles, ina vyumba saba vya kulala, mabafu tisa, swimming pool kubwa.
bey5
bey4
bey3
bey h
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment