Monday, February 23, 2015

MBUNGE NA KUVAA NGUO YA KUBANA

Ya huyu MBUNGE wa Canada na nguo ya ndani inayombana ndani ya Kikao cha Bunge…

1297213432431_ORIGINALKumekuwa na matukio mengi yanayotokea ndani ya Mabunge mbalimbali duniani halafu yanachukua headlines kubwa mtaani na mitandaoni, tumeona ya TZ, Kenya, Afrika Kusini ile juzi wakati Rais Zuma akiwa anahutubia, hii nakupa na wewe uipate kutoka ndani ya Mjengo wa Bunge Canada.
Mbunge Pat Martin naye katoa kali ya mwaka, ile story yake aliyoitoa yani hakuna Mbunge ambaye hakucheka.
Kulikuwa na ishu ya kupiga kura ikiendelea ndani ya Bunge hilo, Mbunge huyo akahojiwa sababu iliyomfanya awe nje ya Jengo wakati zoezi la kura likiendelea, katika kujitetea akajibu kwamba alijikuta akilazimika kutoka nje ya kikao kutokana na nguo ya ndani aliyokuwa ameivaa ilikuwa ikimbana sana hivyo asingeweza kuvumilia kuendelea kukaa ndani ya kikao hicho.
Pat Martin alijitetea kwamba anadhani kilichomponza ni kitu ambacho kimewaponza wengi pia ishu ya kutaka kununua vitu vya bei poa ama kuomba kupunguziwa bei za vitu.
Yeye alinunua nguo hizo za ndani nyingi baada ya kuzikuta zikiuzwa kwa nusu bei, akanunua nyingi bila hata kujua kama zilikuwa zinamtosha size au hapana.
image
Wabunge wakiangua kicheko wakati Mheshimiwa huyo akijieleza.
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia , niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment