Thursday, February 19, 2015

PICHA YA MTU ALIEUWAWA KWA KISU MAREKANI

Picha na taarifa ya mtu wa Nicki Minaj aliyeuwawa kwa visu, huyu mwingine kachomwa pia.

Nicki MinajHawa jamaa wawili wanaoonekana kwenye picha walikua ni sehemu ya timu ya Nicki Minaj, walikwenda sehemu inaitwa Philadelphia Marekani ambapo ni siku mbili tu zimepita toka waingie kwenye mji huo kwa ajili kujiandaa na ziara ya kimuziki ya Nicki Minaj.
Polisi wamesema aliyefariki ni De’Von Pickett, 29, au Day Day anaeonekana kushoto kwenye picha Eric Parker, 27 mwingine aliyejeruhiwa anaendelea vizuri na matibabu.
Kilichotokea ni wao kuchomwa visu kwenye ugomvi uliotokea wakiwa Baa usiku wa Jumanne na rafiki zao ambapo baada ya kuchomwa visu walikimbizwa Hospitali lakini muda mfupi baadae Day Day akawa amefariki.
Nicki Minaj 1Polisi wamesema watamzawadia milioni zaidi ya thelathini na tano mtu yeyote atakaefanikisha kukamatwa kwa Mtuhumiwa aliewachoma visu.

No comments:

Post a Comment