Wednesday, May 20, 2015

BOSS AMFANYIA UKATILI BINTI WAKE WA KAZI

Pale ambapo Bosi anaamua kumfanyia ukatili msichana wake wa kazi baada ya kuibiwa pesa !!

A-silhouette-of-woman-loo-007
 Leo Tena inatoka Dar.. inasikitisha kutokana na tukio ambalo limetokea linahusu msichana mmoja ambaye alifanyiwa ukatili na mwanamke ambaye alikuwa bosi wake wa zamani.
Bosi huyo anadai kuwa msichana huyo aliiba pesa Mil. 2, akawatafuta vijana wawili ambao walimtafuta msichana huyo, walipompata wakampiga na kumuumiza sehemu mbalimbali mwilini.
Watu ambao walimwona msichana huyo akiwa kwenye hali hiyo mbaya na majeraha waliwahoji kuwa ni nini walichomfanyia? Nao wakaamua kuwavamia na kuwapiga waliomfanyia ukatili huo ikiwemo mwanamke aliyedai kuibiwa.
Mzee mwenye nyumba ambapo msichana huyo alikuwa anaishi baada ya kutoroka kwa bosi wake, amesema msichana huyo alikubali kwamba ni kweli alichukua pesa kwa mama huyo na haikuwa mara ya kwanza kufanya wizi wa aina hiyo.

No comments:

Post a Comment