Friday, May 15, 2015

DESMOND TUTU AMSHITAKI MJUU WAKE

Desmond Tutu amshtaki mjukuu wake

Askofu mkuu mstaafu Desmond Tutu
Askofu mkuu mstaafu wa mji wa Capetown na mshindi wa tuzo la Nobel Desmond Tutu pamoja na mkewe wamemshtaki na mashtaka ya uhalifu mjukuu wao.
Katika taarifa kupitia wakfu wa Desmond na Leah Tutu hawakutoa maelezo zaidi ,lakini maafisa wa polisi wa Afrika kusini wamesema kuwa wanachunguza kesi kuhusu uharibifu wa mali kwa makusudi.
Mjukuu huyo Ziyanda Palesa Tutu anatarajiwa kujisalimisha kwa polisi.
Wakfu huo umesema kuwa familia imeshangazwa na kitendo hicho na wanatumai kwamba wataliweka nyuma swala hilo hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment