Friday, May 1, 2015

DROBA ANYAKUA TUZO YA HESHIMA ENGLAND

Tuzo nyingine ya heshima aliyopewa Didier Drogba…

droooMbali na uwezo wake mkubwa wa kumiliki mpira uwanjani, Didier Drogba raia wa Ivory Coast amekuwa na mchango mkubwa katika shughuli za kijamii ambazo ambazo amekuwa akishiriki ndani ya nchi yake na Afrika kwa ujumla.
Uongozi wa ligi kuu ya England umeona ni vyema ukaonyesha kuridhishwa na kazi zake na kuamua kumpa tuzo kutokana na mchango wake mkubwa wa kuhamasisha soka la vijana Afrika kupitia michango yake na uamuzi wake wa kufungua Didier Drogba Foundation ambayo itakuwa ikifanya kazi ya kuwasaidia wenye matatizo.
Staa huyo wa soka wa Chelsea amepewa heshima hiyo kubwa na uongozi huo kama sehemu ya kumpongeza kwa kazi nzuri za kijamii anazofanya.
Tayari Drogba amejenga hospitali kubwa ya kisasa nchini kwao Ivory Coast.

No comments:

Post a Comment