Friday, May 1, 2015

WATUHUMIWA WA MALALA WAFUNGWA MAISHA JELA

Hii ni hukumu ya waliompiga risasi mwanaharakati mdogo Pakistan

malala-yousafzai-nobel-prize-winnerJina la Malala Yousafzai liliwahi kukaa kwenye vichwa vya habari vya Kimataifa mwaka 2012 kutokana na tukio la msichana huyo kupigwa risasi akiwa ndani ya basi lao la shule.
Malala alikuwa na umri wa miaka 15 wakati huo, tukio la kupigwa risasi linahusishwa na ishu yake kujihusisha na harakati za kudai haki za watoto hasa wa kike kwenye suala la elimu.
Mwaka 2014 jina lake likarudi tena kwenye headlines baada ya kupewa Tuzo ya amani ya Nobel, kilichoripotiwa leo kinarudisha kumbukumbu ya tukio la kupigwa risasi mwaka 2012.
Watuhumiwa 10 ambao walikamatwa kwa kesi ya kuhusika na tukio la kumpiga risasi Malala wamehukumiwa kifungo cha maisha jela.
Malala Yousafzai lying in hospital bed
Malala baada ya shambulio akiwa Hospitali.
Baada ya kupigwa risasi Malala alifanyiwa upasuaji Uingereza, baada ya hali yake kukaa sawa ameendelea na kampeni zake Kimataifa.
Malala ni mmoja ya watu wenye umri mdogo na wana rekodi kubwa.. wakati anatunukiwa Tuzo ya Nobel alikuwa na umri wa miaka 17 tu.
Nobel Peace Prize laureate Malala Yousafzai poses with her medal during the Nobel Peace Prize awards ceremony at the City Hall in Oslo December 10, 2014. Pakistani teenager Malala Yousafzai, shot by the Taliban for refusing to quit school, and Indian activist Kailash Satyarthi received their Nobel Peace Prizes on Wednesday after two days of celebration honouring their work for children's rights. REUTERS/Cornelius Poppe/NTB Scanpix/Pool   (NORWAY  - Tags: SOCIETY CIVIL UNREST TPX IMAGES OF THE DAY) NORWAY OUT. NO COMMERCIAL OR EDITORIAL SALES IN NORWAY.
Malala alipotunukiwa Tuzo ya Nobel
Hutopitwa na habri yoyote na kuwa karibu nami nitakusogezea muda na wakati wowote hapa hapa tangakumekuchablog.com

No comments:

Post a Comment