Thursday, May 7, 2015

WENGI WAMUUNGA MKONO EDEBAYOR

Jinsi mastaa wa Afrika walivyomuandikia Adebayor kwenye mgogoro wa familia

LONDON, ENGLAND - FEBRUARY 09:  Emmanuel Adebayor of Tottenham Hotspur reacts during the Barclays Premier League match between Tottenham Hotspur and Everton at White Hart Lane on February 9, 2014 in London, England.  (Photo by Shaun Botterill/Getty Images)
Siku chache baada ya mshambuliaji wa kimataifa wa Togo na Tottenham Hotspurs Emanuel Sheyii Adebayor kufichua siri kadhaa nzito za ugomvi na familia yake, mastaa kadhaa wa Afrika wamemuunga mkono kwenye hii ishu.
Moja kati ya mapacha wanaoiunda P-Square Peter amemuunga mkono Adebayor ambapo amemsifu kwa ujasiri wake na jinsi alivyojitokeza kuwa muwazi na kutoa yanayomsibu maishani mwake.
Mwanamuziki Peter wa kundi la P-Square amemuunga mkono Adebayor kwa kitendo chake cha kufichua mgogoro ulioko kati yake na familia yake .
Mwanamuziki Peter wa kundi la P-Square amemuunga mkono Adebayor kwa kitendo chake cha kufichua mgogoro ulioko kati yake na familia yake .
Peter amemuandikia Adebayor kwa kuandika ‘Ukweli ni kwamba hakuna mtu anayekudai lolote , familia yako inapaswa kuona fahari kuwa na mtoto kama wewe na si kinyume chake ‘.
Nyota wa zamani wa Arsenal Emmanuel Frimpong kwa upande wake aliandika kwenye ukurasa wake wa twitter ambapo amesema kuwa baada ya kusoma kilichomsibu Adebayor anashukuru Mungu kwani familia yake ni kila kitu kwake .
Nyota wa Chelsea na mshambuliaji wa zamani wa Ivory Coast Didier Drogba naye alionyesha kumuunga mkono na amemuombea kwa Mungu na anajua ipo siku familia ya Adebayor itarudi katika msingi wa familia zote ambao ni Upendo.
Nyota wa Chelsea Didier Drogba naye amejitokeza kumpa 'Support' Adebayor katika mgogoro wake na familia yake.
.
Didier Drogba ni mmoja kati ya watu ambao wamekuwa karibu na Adebayor katika kipindi hiki kigumu na inasemekana kuwa alizungumza na Adebayor saa chache kabla ya kuandika waraka mrefu kwenye mtandao wa Facebook .
Adebayor amefichua mgogoro mkubwa ulioko baina yake na ndugu zake pamoja na mama yake mzazi ambapo amesema kuwa kilichomfanya afanye hivyo ni kutoa fundisho na picha halisi ya jinsi ambavyo familia za Afrika zina shinikizo kwa vijana waliofanikiwa.
Dada wa Adebayor anayefahamika aitwae Lucia amejibu mapigo ya waraka ulioandikwa na Adebayor ambapo amesema kuwa kila kilichoandikwa na staa huyu wa soka ni uongo na kwa sasa familia yake haimuhitaji.
Kwa habari na matokeo kemkem ni hapa hapa tangakumekuchablog

No comments:

Post a Comment