Friday, February 10, 2017

DANKANI MWAMBA AWALAUMU WACHEZAJI WAKE



Tanga, KOCHA Mkuu wa timu ya Kwamdolwa FC ya Korogwe Tanga inayoshiriki ligi daraja la nne ngazi ya Mkoa, Dankan Mwamba ameitupia lawama timu yake  kwa kukubali kipigo cha mabao 3, 1 kutoka kwa timu ya Majengo FC ya Tanga.
Akizungumza baada ya kumalizika mchezo huo uwanja wa Mkwakwani jana, Dankan, alisema wachezaji wake walicheza mchezo mbovu na kudai kuwa sivyo alivyowafundisha kucheza.
Alisema kipigo hicho ni lawama kuanzia kipa hadi mchezaji wa mwisho na kuwataka wachezaji wake kubadilika haraka vyenginevyo kikosi chake atakipangua upya.
“Sijafurahishwa na uchezaji wa wachezaji wangu ni tofauti kabisa na mafundisho ambayo nimekuwa nikiwaelekeza wakati wa mazoezi” alisema Dankan na kuongeza
“Wakati wa mazoezi kila mmoja ukimuangalia unamuona bora na kushindwa nani kumuanzisha, lakini wakati wa mechi uwanjani ni tofauti kabisa na kubaki kuumwa na kichwa” alisema
Aliwataka wachezaji wake kukichukulia kipigo hicho kama changamoto ya kupata matokea mazuri katika michezo iliyoko mbele yao na kusema kuwa wanarejea Korogwe na kutokuwa na lakuwambia washabiki wa timu yake.
Kwa upande wake kocha wa Majengo FC ya mjini Tanga, Shaban Bakari, amesema ushindi huo wa mabao 3 umewatia mori wachezaji wake wakiwemo wakufunzi wa timu hiyo.
“Kila siku hufurahi  kupata pointi tatu lakini leo nimepata pointi tatu na magoli matatu jambo ambalo linanifanya niweze kutembea kifua mbele mitaa” alisema Bakari
Aliwataka wachezaji wake kutobweteka na ushindi huo badala yake kuongeza kasi ya mazoezi na bidii uwanjani ili kuweza kupata matokeo mazuri mfululizo.
                                          Mwisho


Mchezaji wa Kwamdolwa FC, Ali Vote (5) akigombea mpira na mchezaji wa Majengo FC wakati wa mchezo ligi daraja la nne ngazi ya Mkoa uwanja wa Mkwakwani juzi, Majengo iliibuika na ushindi wa mabao 3, 1.

No comments:

Post a Comment