Monday, February 27, 2017

MKUU WA WILAYA YA MUHEZA AWAPIGA MSASA WAJASIRIAMALI WANAWAKE TANGA



Tanga, MKUU wa Wilaya ya Muheza, Mwanasha Tumbo amewataka Wajasiriamali wanawake Tanga kulitumia soko la pamoja la Afrika Mashariki kwa kutafuta masoko na kuacha kutegemea masoko ya ndani.
Aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa  Jukwaa la Kuwawezesha Wanawake Kiuchumi Mkoani hapa jana, Tumbo alisema soko hilo endapo Wajasiriamali nchini wangelitumia wangelienuka kiuchumi.
Alisema kazi za mikono ziko na soko kubwa ndani na nje ya nchi hivyo kuwataka kutambua na kuwa tayari kuyafikia masoko kama ilivyo kwa wenzao ndani ya jumuiya hiyo.
“Niwambie wajasiriamali wenzangu kwani hata mie pia ni mjasiriamali ila nadhani niko tofauti na nyie, lilipofunguliwa tu soko la pamoja sikukumbatia masoko ya ndani” alisema Tumbo na kuongeza
“Nilisafiri na biashara zangu mkononi bila woga na kweli bidhaa zangu zikawa bora zaidi na kupata wateja wengi ikafikia wao kunifuata kwangu” alisema
Aliwakumbusha  Wajasiriamali hao kulitumia vyema soko la pamoja kama ilivyo kwa wenzao jambo ambalo litawawezesha kuwa wajasiriamali wakubwa na wa Kimataifa.
Kwa upande wake Mjasiriamali kikundi cha Twaweza, Aziza Said, alisema wajasiriamali wengi wa vikundi vyao haviendelei kutokana na kukosa mikopo ya kujiendeleza.
Alisema kuna baadhi ya taasisi za fedha zinaweka masharti magumu jambo ambalo limekuwa kukwazo cha vikundi vyao kuendelea hivyo kuitaka Serikali kusaidia ili kuweza kujikwamua.
“Mikopo imekuwa na masharti magumu sana na kuwa chanzo cha baadhi ya vikundi kusambaratika na wengine kuhasimiana” alisema Aziza
Ameitaka Serikali Mkoani hapa kuwa mlezi wa vikundi vya wanawake kuhakikisha wanasonga mbele katika kujikwamua na maisha jambo ambalo litaepuka na viashawishi vya nje.
                                              






No comments:

Post a Comment