Monday, February 6, 2017

LUKUVI ATEKELEZA AGIZO LA WAZIRI MKUU KUMALIZA MGOGORO WA MPAKA KILINDI, KITETO


Tanga, WAZIRI wa Ardhi, Nyumba, Maendeleo na Makaazi, William Lukuvi, amesema mgogoro wa mpaka kati ya Kilindi kwa  Tanga na Kiteto kwa Mkoa wa Manyara utapatiwa ufumbuzi karibuni,
Akizungumza katika kikao na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shighella na Joel Bendera Mkuu wa Mkoa wa Manyara pamoja na Wakuu wa Wilaya na Madiwani wa Kilindi na Kiteto, Lukuvi amesema kikao hicho ni agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Amesema mgogoro huo wa mpaka uko muda mrefu na  kusema kuwa awamu hii ya tatu ndio ya mwisho na hakutakuwa na mpaka mwengine zaidi ya awali wa mwaka 1961 ambao utaboreshwa kwa kuwekwa alama za kudumu zenye kuonekana kwa mujibu wa makubaliano ya pande zote mbili.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shighella, amesema kupatikana kwa ufumbuzi wa mpaka huo kutaondosha vitisho na hofu ya wakulima na wafugaji wa pande mbili hizo.
Nae Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Joel Bendera, amesema Serikali ya Mkoa wake itatoa ushirikiano ili kumaliza mgogoro huo ambao umedumu kwa muda mrefu.
Mgogoro wa mpaka kati ya Kilindi kwa Mkoa wa Tanga na Kiteto kwa Mkoa wa Manyara umedumu kwa muda mrefu na kupelekea baadhi ya nyakati  kuzuka hali ya Sintofahamu  ya wakulima na wafugaji.
Hivi karibuni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitembelea Wilaya mbili hizo Kilindi kwa Mkoa wa Tanga na Kiteto kwa Mkoa wa Manyara  na kusikiliza changamoto mbalimbali na mwisho kuagiza ufumbuzi wa mpaka kati ya Kilindi na Kiteto upatiwe ufumbuzi haraka






No comments:

Post a Comment