Tuesday, February 7, 2017

WABUNGE WA UPINZANI WATOKA NJE BUNGENI

Wabunge wa Upinzani wametoka nje ya ukumbi wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania baada ya kutoridhishwa na maamuzi ya Naibu Spika Dr. Tulia.
Inaripotiwa kwamba Naibu Spika Dr. Tulia aliamuru kutolewa nje kwa Mbunge Halima Mdee na mwenzake waliopaza sauti ndani ya bunge baada ya Naibu spika kukataa mwongozo wa kujadili sababu za kukamatwa kwa Mbunge Tundu Lissu jana.
Baada ya amri ya kuwatoa nje Halima Mdee na mwenzake inaripotiwa na Wabunge wengine wa upinzani wakachukua uamuzi wa kutoka nje.

No comments:

Post a Comment