Friday, February 10, 2017

HADITHI, ALIYEEMUUA MCHUMBA WANGU SEHEMU YA 30

HADITHI
ALIYEMUUA MCHUMBA WANGU
ILIPOISHIA 
“Nina hospitali yangu. Ilikuwa ni ya mume wangu, alipofariki nikabaki nayo mimi”
 
“Wewe ni daktari?’
 
“Hapana. Mume wangu ndiye aliyekuwa daktari”
 
“Hata mimi fani yangu ni ya udaktari”
 
“Daktari wa nini?”
 
“Mimi ni daktari bingwa wa upasuaji”
 
Mwana akamtazama Kweka usoni.
 
“Sikukutambua. Unafanya kazi aliyokuwa akifanya mume wangu”
 
“Hivi sasa niko kwenye likizo, ndio sababu nimekuja huku”
 
“Ninashukuru sana kwa kunifahamisha hilo”  
 
SASA ENDELEA 
“Nashukuru umenisaidia, nilikuwa nimechanganyikiwa” Mwana akamwabia Kweka wakati anaendesha.
 
“Matukio ya aina ile yanachanganya akili lakini inatakiwa uwe makini na uchukue hatua za haraka haraka ili kuokoa maisha”
 
“Ni kweli. Nitampeleka kwenye hospitali yangu”
 
“Wewe una hospitali?”
 
“Nina hospitali yangu. Ilikuwa ni ya mume wangu, alipofariki nikabaki nayo mimi”
 
“Wewe ni daktari?’
 
“Hapana. Mume wangu ndiye aliyekuwa daktari”
 
“Hata mimi fani yangu ni ya udaktari”
 
“Daktari wa nini?”
 
“Mimi ni daktari bingwa wa upasuaji”
 
Mwana akamtazama Kweka usoni.
 
“Sikukutambua. Unafanya kazi aliyokuwa akifanya mume wangu”
 
“Hivi sasa niko kwenye likizo, ndio sababu nimekuja huku”
 
“Ninashukuru sana kwa kunifahamisha hilo”  
 
“Na ni kwanini umeamua kumpeleka kwenye hospitali yako binafsi?” Alphonce akamuuliza Mwana.
 
“Kama nitampeleka katika hospitali ya serikali, itabidi niripoti polisi na sitapenda kesi hii ifike polisi”
 
“Unataka mmalizane kienyeji?”
 
“Inatosha”
 
Baada ya hapo wakawa kimya hadi walipofika katika hospitali hiyo. Ilikuwa hospitali kubwa kiasi iliyokuwa na majengo ya kupendeza na ya kisasa. Mwana alisimamisha gari kwenye eneo la maegesho ambalo lilikuwa na magari kadhaa.
 
Alifungua mlango akashuka  na kwenda kuwaita wauguzi ambao walifika na machela, wakambeba yule mwanamke na kuingia naye ndani ya majengo ya hospitali hiyo.
 
“Twende” Mwana alimwambia Alphonce.
 
Waliingia katika mlango wa hospitali hiyo wakatokea sehemu ya mapokezi ambayo waliipita na kutokea katika ukumbi mwembamba wa hospitali hiyo.
 
“Nisubiri” Mwana alimwambia Alphonce alipofungua mlango wa chumba cha madaktari na kuingia ndani. Baadaye kidogo alitoka akiwa na madaktari watatu mmoja akiwa mwanamke.
 
“Twende” akamwambia Alphonce.
 
Wakaelekea katika chumba cha matibabu. Wale wauguzi waliokuwa wamemchukua yule mwanamke walikuwa wakimuingiza kwenye chumba hicho.
 
“Huyu ni rafiki yangu na pia ni daktari kutoka Tanzania” Mwana aliwambia wale madaktari.
 
Madaktari hao wakasalimiana na Alphonce.
 
Walipofika kwenye mlango wa chumba cha matibabu waliingia wote. Mwana alikuwa ameshawaeleza madaktari hao kuwa alikuwa amemgonga mwanamke huyo ambaye alikuwa akiendelea kutapatapa.
 
Mwanamke huyo alilazwa na kuanza kushughulikiwa. Mwana na Alphonce walikuwa wamesimama pembeni mwa chumba hicho wakitazama.
 
Madaktari hao waligundua kuwa damu iliyokuwa ikimtoka mwanamke huyo ilikuwa ikitoka katika sehemu yake ya kike. Kwa vile ilikuwa ni nyingi iliwachanganya na kutojua ilikuwa inatokea sehemu gani.
 
Kwa karibu saa nzima walikuwa wakijaribu kuizuia bila mafanikio. Wakati wakiendelea na jitihada zao waliagiza awekewe damu nyingine.
 
“Unaweza kutusaidia?”Mwana alimuuliza Alphonce.
 
“Naweza”
 
“Tusaidie”
 
Kweka aliletewa koti la udaktari akaomba apatiwe mipira ya kuvaa mikononi.
 
Alipopatiwa mipira hiyo aliliminyaminya tumbo la mwanamke huyo kisha akamtazama Mwana.
 
“Huyo mwanamke anaujauzito ambao umeharibika, anahitajika kufanyiwa operesheni kuokoa maisha yake”
 
Wale madakatari waliokuwepo pale wakatazamana. Hawakuwa wamefikiria jambo hilo.
 
Alphonce akaagiza vifaa vya kufanyia operesheni. Vifaa hivyo vilipoletwa alimpasua tumbo yule mwanamke. Alikitoa kichanga cha miezi mine kilichokuwa kimepoteza uhai kutokana na ajali iliyotokea. Kichanga hicho ndicho kilichosababisha kuvuja kwa damu.
 
Alphonce alimsafisha na kumuweka sawa kisha akaanza kumshona. Alipomaliza alimwambia Mwana.
 
“Nafikiri tatizo lake limekwisha. Sasa mnaweza kumtibu michubuko”
 
Dakika chache baadaye mwanamke huyo alikwenda kuwekwa katika chumba cha peke yake. Alphonce alivua koti la udaktari akampa Mwana.
 
“Unadhani akizinduka atajisikia vizuri?” Mwana akamuuliza Alphonce kwa wasiwasi.
 
“Bila shaka yoyote”
 
“Tuombe Mungu”
 
Wakati huo walikuwa wameketi kwenye chumba cha mapumziko. Mwana akatazama saa yake na kumwambia Alphonce.
 
“Nimepoteza muda wako mwingi’
 
“Hakuna tatizo”
 
“Kwa hiyo nikurudishe hotelini?”
 
“sawa”
 
Walitoka na kupanda gari. Walifika hotelini hapo na kukaa kwenye mkahawa.
 
“Wakati ule nilikuwa nakuja kunywa supu” Mwana akamwambia Alphonce.
 
“Unawza kunywa sasa hivi, nadhani moyo wako umetulia kidogo”
 
Mwana akaagiza supu na chapati mbili.
 
“Wewe je?”
 
“Mimi tayari”
 
“Ongeza”
 
“Hapana, ni mpaka saa saba”
 
Mwana alipoletewa supu na chapatti alianza kunywa.
 
“Yule mwanamke ningempeleka hospitali ya serikali angekufa” Mwana alimwambia Alphonce.
 
“Kama wasingelichunguza kwa makini tatizo lake, angeweza kupoteza uhai”
 
“Lakini kwa jinsi ulivyomshughulikia una uhakika kuwa amepona?”
 
“Yule ameshapona, sina wasiwasi naye”
 
“Utanipatia namba yako ya simu ili nikupigie kukujulisha hali yake”
 
“Nitakupatia, namba yangu ni ya kimtaifa ndiyo ninayotumia hata nikiwa Tanzania”
 
“Ni ngapi?”
 
Alphonce alimpa namba yake. Mwana naye alimpa ya kwake.
 
Baada ya kumaliza kunywa supu, Mwana aliondoka na kumuacha Kweka.
 
Saa saba mchana wakati Kweka anakula chakula, Mwana alimpigia simu.
 
“Vipi huko?” Alphonce akamuuliza.
 
“Nimefurahi. Madaktari wangu wameniambia yule mwanamke amezinduka na anazungumza” Sauti ya Mwana ikasikika kwenye simu.
ITAENDELEA KESHO hapahapa usikose

No comments:

Post a Comment