Monday, February 20, 2017

DC, MUHEZA AIKUMBUSHA JAMII KUWAKUMBUKA WAZEE



Muheza, Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mwanasha Tumbo ameitaka jamii kuwasaidia watu wasiojiweza na kuwapa misaada ili kuweza kuishi katika mazingira mazuri kama wengine.
Akizungumza katika tafrija ya  wazee 58 waliopata tiba ya Upasuaji wa mtoto wa jicho uliofanywa na madaktari bingwa  kutoka taasisi ya Medewell  Health Centre ya Kibaha Mkoani Pwani, Tumbo amesema wazee wanahitaji uangalizi maalumu.
Ameseme mashirika na taasisi za watu binafsi wanatakiwa kuiga mfano wa Medewell ili kuhakikisha tatizo la macho kwa wazee na magonjwa mengine yanatokomezwa.
Akitoa shukrani zake, Mganga Mfawidhi kituo cha Afya cha Ubwari Health Centre, Rymond Mhina, amesema matibabu yaliyofanyika yalienda salama kama ilivyokusudiwa mbali ya changamoto ndogondogo kutoka kwa wazee.
Alisema baadhi ya wazee walikuwa woga na kudhani kuwa matibabu hayo yangewaweka katika mazingira mengine tofauti ambapo wengi walifurahia na kuona kama zamani.
Akizungumza mara baada ya kufanyiwa matibabu hayo, Lea Stivin mkazi wa Majengo ameishukuru taasisi hiyo na kusema kuwa kuna wazee wengi ambao wanaugonjwa wa macho.
Alisema kupitia kwao wanaweza kujitokeza kundi jengine hivyo kulitaka shirika hilo kuwa na moyo wa kusaidia na kuwataka wengine kuiga mfano huo.
                                                        
Mzee Rajab Hassan (CHINI)  mkazi wa Bwembwera akielezea matibabu ya upasuaji wa mtoto wa jicho aliofanyiwa na taasisi ya Medewell Charitable Health Centre  kituo cha Afya Ubwari Wilayani Muheza Mkoani Tanga ambapo wazee 58 walifanyiwa upasuaji na kuruhusiwa kurejea majumbani.



Mkuu wa Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga, Mwanasha Tumbo, akimvisha miwani, Mwajuma Omari  mara baada ya kufanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho uliofanywa na Taasisi ya Medewell Charitable Health Centre kutoka Kibaha Mkoani Pwani .

No comments:

Post a Comment