Friday, February 10, 2017

KOCHA WA SAHARE FC YA TANGA ADAI GOLI LA DAKIKA 90 NI MIUJIZA YA MUNGU



Tanga, KOCHA Mkuu wa timu ya Sahare FC inayoshiriki ligi daraja la nne ngazi ya Mkoa, Joseph Lazaro, amesema timu yake kupata bao la kusawazisha dakika za nyongeza dhidi ya Korogwe FC ni miujiza ya Mungu.
Akizungumza  na vyombo vya habari mara baada ya kumalizika mchezo huo, Lazaro alisema alivyoichukulia timu hiyo ni tofauti walivyouanza mchezo.
Alisema alivyojua timu za mashamba haziwezi kufua dafu kwa timu za mjini lakini kwa timu ya Korogwe haikuwa hivyo bali kuanzia mwanzo wa mchezo hadi kipenga cha mwisho walikuwa bora zaidi yao.
“Dah kwa kweli nilivyowachukulia wapinzani wetu ni tofauti na ilivyokuwa imani yangu jogoo wa shamba hawiki mjini lakini kumbe sio hivyo wametuendesha puta” alisema Lazaro na kuongeza
“Kipindi cha pili kidogo tulionyesha matumaini ya kutafuta magoli lakini nao wenzetu  walikuwa  wakilinda goli, ila nisema goli lile la kuwaswazisha dakia za nyongeza  ni miujiza ya Mungu
Amewataka wachezaji wake kujifunza kwa mchezo huo kwa kufanya mazoezi kwa bidii ili kufanya vizuri katika  michezo iliyoko mbele yao na kuweza kujiweka nafasi nzuri.
Kwa upande wake, kocha wa Korogwe FC, Salim Juma Makame, amewataka wachezaji wake kujilaumu kwa kushindwa kulinda goli na kuruhusu Sahare kusawazisha dakika za nyongeza.
Alisema kwa mchezo huo atafanya mabadiliko madogo katika safu ya ulinzi na ushambuliaji na kubadilisha mfumo wa uchezaji badala wa sasa wa kupiga mipira mirefu.
“Dakika za majeruhi wachezaji wangu walikuwa hawaelewani uwanjani na kucheza fyongo na kupelekea kuruhusu goli dakia za mwisho” alisema Makame
Aliwataka wachezaji wake  kusahau matokeo hayo na kuangalia mchezo ambao uko mbele yao na kuweza kufanya vizuri mwanzo mwisho.
                                              



 Kiungo wa Sahare FC, Ali Salim (chini) akigombea mpra na mchezaji wa Korogwe FC, Martin Thomas wakati wa mchezo ligi daraja la nne ngazi ya Mkoa uwanja wa Mkwakwani juzi, Timu hizo zilitoka suluhu kwa kufungana bao 1, 1.
Mshambuliaji wa Korogwe FC (8), James Semi akigombea mpira na kiungo wa Sahare FC, Abdull Mgaya wakati wa mchezo ligi daraja la nne ngazi ya Mkoa uwanja wa Mkwakwani juzi, Timu hizo zilitoka suluhu kwa kufungana bao 1 , 1.

No comments:

Post a Comment