Tuesday, February 7, 2017

WATUHUMIWA 13 WA MADAWA YA KULVYA MAHAKAMANI

Washukiwa 13 mahakamani kwa tuhuma za biashara ya mihadarati Tanzania

Washukiwa 13 mahakamani kwa tuhuma za biashara ya mihadarati Tanzania
Washukiwa 13 mahakamani kwa tuhuma za biashara ya mihadarati TanzaniaWashukiwa 13 wakiwemo wasanii mashuhuri wamefikishwa mahakamani mjini Dar es Salaam , baada ya ombi maalamu la polisi kutaka wawekwe chini ya uangalizi kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Watuhumiwa hao wameamriwa na mahakama wawe chini ya uangalizi wa polisi kwa mwaka mmoja ambapo pia wametakiwa kujidhamini kwa bondi ya shilingi milioni 10 za Tanzania sawa na dola 4000.
Polisi  wamekuwa wakiwashikilia watu zaidi ya 10 wakiwemo wasanii maarufu na polisi waliotajwa na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kuhusika na biashara ya dawa za kulevya.
Miongoni mwa wale waliohojiwa, alikuwemo msaanii maarufu na miss Tanzania wa mwaka 2006, Wema Sepetu, aliyeitikia wito wa polisi pamoja wasanii wenzake kufika kwa mahojiano.

No comments:

Post a Comment