Tuesday, February 28, 2017

MEYA JIJI LA TANGA APIGA MARUFUKU UVAAJI WA JEANZ NA NGUO AMBAZO HAZINA STAHA



Tanga, MEYA wa jiji la Tanga, Mustapha Mhina, amepiga marufuku uvaaji wa suruali aina ya jeanzi wakati wa vikao vya baraza na kuwataka kuheshimu vyenginevyo kanuni za baraza kwa kuwatoa nje.
Akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani jana, Mhina alisema ni marufuku kuvaa suruali aina ya jeanzi pamoja na mavazi mengine ambayo hayana staha ndani ya baraza.
Alisema kwa muda mrefu amekuwa akioona tabia hiyo na kuivumilia jambo ambalo amelichunguza hakuna mabadiliko hivyo kanuni za baraza zitafanya kazi bila ya kuonea mtu hutuma wala sura.
“Waheshimiwa madiwani mwisho leo kumuona diwani amevaa suruali aina ya jeanzi au mavazi ambayo hayana staha si kwa wanawake wala wanaume” alisema Mhina na kuongeza
“Hiki ni chombo kinatakiwa kuheshimiwa na kila mjumbe wa baraza hili natoa angalizo mapema kikao kijacho kabla ya kuanza kwa baraza nafanya ukaguzi” alisema
Alisema kuanzia sasa atakuwa mkali kwa kila jambo ambalo ataliona haliko sawa ndani ya baraza ikiwemo kufika kwa wakati ndani ya baraza na utoro ambao hautakuwa na taarifa.
Kwa upande wake Diwani wa kata ya Maweni , Joseph Collivas (CCM) amewataka wajumbe wa baraza la madiwani kutoa kero za wananchi katika maeneo yao na kuyapatia ufumbuzi wa haraka.
Alisema kuna changamoto nyingi katika maeneo ambayo madiwani wanawakilisha lakini hadi muda wa sasa hakuna hatua zozote ambazo zimepatiwa ufumbuzi ikiwemo mrefeji wa maji eneo la stendi kuu ya mabasi ya Kande ambayo hayana uelekeo.
“Madiwani wenzangu hebu tujadilini kero za wananchi ambao wametuchagua na kuyapatia ufumbuzi, kila mmoja kwake kuna kero kama sio dampo kuna migogoro iwe ya mipaka au ya viwanja” alisema
Aliwataka madiwnai hao kuhakikisha wanavitumia vikao hivyo kwa manufaa kwa wananchi bila kuangalia chama kwa madai kuwa kinachotakiwa ni maendeleo ya wananchi.
                                                     Mwisho
.


Meya wa jiji la Tanga, Mustafa Mhina (kushoto) akijadiliana jambo na Mkurugenzi wa jiji la Tanga, Daudi Mayeji wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani

No comments:

Post a Comment