Monday, February 13, 2017

WAHAMIAJI HARAMU 25 WENYE ASILI YA ETHOPIA WAKAMATWA WAKIELEKEA TUNDUMA



Tanga, JESHI la Polisi Mkoani Tanga limewakamata wahamiaji haramu 25 wenye asili ya Ethopia wakiwa wamefichwa kwenye gari aina   FUSO wakitokea Rombo Mkoani Kilimanjaro wakisafirishwa kuelekea Tunduma.
Wahamiaji hao ambao pia walikuwemo wanawake watano walikutwa wakiwa wamechoka kwa njaa huku baadhi yao wakilalamika kukaa muda mrefu kwenye gari na kukosa huduma muhimu ikiwemo maji ya kunywa.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga, Benedict Wakulyamba, amesema tukio hilo lilitokea juzi saa 4 usiku katika kizuizi cha polisi Mombo.
Amesema kwa sasa wanawashikilia pamoja na dereva wa gari hilo na kondakta wake na mara baada ya uchunguzi kukamilika watapelekwa mahakamani  kujibu tuhuma zinazowakabili.
Katika tukio jengine jeshi la polisi limekamata silaha nne aina ya Gobore Wilayani Kilindi ambazo zilikuwa zikitumika katika uhalifu.
Silaha hizo zimekamatwa wakati wa msako unaofanywa na jeshi hilo baada ya taarifa za kuwepo kwa watu ambao wanasadikiwa kuwa majambazi kuendesha vitendo vya kihalifu.
                                                   







No comments:

Post a Comment