Tuesday, February 28, 2017

KENYA KUCHEZA NA HULL CITY YA UINGEREZA

Uwanja wa Hull City nchini UingerezaTimu inayoshirikisha wachezaji wa Kenya kutoka ligi ya soka ya taifa hilo Watacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Klabu ya Uingereza Hull City.
Mechi hiyo inayofadhiliwa na SportPesa- kampuni ya kamare kutoka Kenya ilioshinda haki ya kuifadhili timu hiyo ya Uingereza kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.
Timu ya Kenya yenye wachezaji 18 imepiga kambi katika maeneo ya Kaskazini mwa Uingereza tangu wiki iliopita ikijifunza mbinu tofauti za soka ya kulipwa.
Siku ya Jumapili Hull City walicheza dhidi ya Burnley ambapo walitoka sare ya 1-1.
Kocha wa timu ya taifa ya Kenya Stanley Okumbi anasema kuwa wachezaji wa Kenya wamenufaika sana na ziara hiyo.

No comments:

Post a Comment