Saturday, February 11, 2017

ARSENAL YAWALIWAZA WASHABIKI WAKE, YAIBAMIZA HULL CITY MABAO 2

Alexi Sanchez akifunga mkwaju wake wa penaltiAlexis Sanchez alifunga mara mbili na kuisaidia Arsenal kuishinda Hull City 2-0 katika uamuzi wa refa uliodaiwa kuwa na utata.
Arsenal ilikuwa ikicheza vyema wakati mpira wa shambulio ulipogonga mkono wa Alexi Sanchez na kuingia katika dakika ya 34.
Sanchez aliongeza bao la pili kupitia mkwaju wa penalti uliotolewa katika dakika za ziada baada ya Sam Clucas kutolewa nje kwa kushika kichwa cha Lucas Perez kilichokaribia kuingia katika goli.
Hector Bellerin na Sanchez wote walishindwa kufunga awali huku Mesut Ozil akipiga juu.
Mshambuliaji wa Hull City Oumar Niasse alikuwa na nafasi nzuri lakini kichwa chake na shambulio lake likaokolewa na kipa Petr Cech.

No comments:

Post a Comment