Saturday, January 31, 2015

MANCHESTE YALIPIZA KISASI KWA LECEISTER CITY

Je Man U wameweza kurudisha kisasi kwa Leceister? Cheki matokeo hapa

IMG_1311-1.PNG
Kumbukumbu za mchezo wao uliopita – Louis Van Gaal anasema ni kitu ambacho angependa kukisahau, wakiwa wanaongoza kwa magoli 3 mechi ikaishia kwa kufungwa 5-3 na Leicester City.
Leo hii miezi takribani minne tangu mechi hiyo ya kwanza ya EPL kuchezwa, Leceister walisafiri mpaka jijini Manchester kwenda kucheza na Man United.
Mchezo huo uliopigwa katika dimba la Old Trafford jana umemalizika kwa Louis Van Gaal kuiongoza United kuweza kulipa kisasi kwa kuifunga Leceister kwa magoli 3-1.
Magoli ya United yalifungwa na Van Persie, Radamel Falcao na moja la kujifunga kwa Leceister wenyewe.
Mpaka timu hizo zinaenda mapumziko United walikuwa wanaongoza 3-0.
Kipindi cha pili United walipunguza kasi na Leceister wakajaribu kufanya maajabu ya kusawazisha magoli na hata kupata ushindi kabisa lakini siku haikuwa yao – wakaishia kupata goli moja tu lilofungwa na Wasilewski.
MANCHESTER UNITED (4-1-2-1-2): De Gea 6; Valencia 7 (Mata 77, 6), Jones 6.5, Rojo 7, Shaw 7; Blind 7.5; Rooney 7, Januzaj 6.5; Di Maria 7; Van Persie 8 (McNair 68, 6), Falcao 7.5 (Wilson 80, 6)
Subs not used: Valdes, Smalling, Herrera, Fellaini
Goal: Van Persie 27, Falcao 32, Morgan OG 44
LEICESTER (4-4-2): Schwarzer 6; Simpson 5, Wasilewski 6.5, Morgan 5; De Laet 6; Vardy 5 (Cambiasso 46, 6), Drinkwater 5, King 6, Schlupp 5; Ulloa 5 (Nugent 62, 6), Kramaric 5 (Albrighton 62, 6.5)
Hutopitwa na habari yoyote mtu wangu, niko tayari kukutumia kila kinachinifikia kupitia, www.tangakumekucha.blogspot.com

No comments:

Post a Comment