Monday, January 26, 2015



Kumekuchablog
Tanga,ABIRIA wanaotumia uwanja wa ndege wa Majanimapana Tanga, jana  walilazimika kusubiria zaidi ya masaa matatu baada ya kuzuka moto mkubwa katikati ya uwanja na kuchukua masaa 13 kuzimwa kwa kusaidiana na wanafunzi wa Chuo cha Anga cha Kijeshi.
Akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake, Kaimu kamanda wa polisi Mkoa wa Tanga, Juma Ndaki, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 8 mchana baada ya wafanyakazi wa uwanja wa ndege kuona moto katika nyasi za uwanja sehemu ya kurukia ndege.
Alisema moto huo ulidumu kwa zaidi ya masaa matatu  na kulazimika kusitisha huduma za kutua na kuruka ndege jambo ambalo liliathiri huduma za usafiri kwa wasafiri wa kisiwani Pemba na Unguja.
“Wafanyakazi wa uwanja wa ndege waliona moshi mkubwa katika nyasi za katikati ya uwanja eneo la kurukia ndege----moto ule ulikuwa ukisambaa kwa kasi na kuja eneo la jengo ambako pia kuna ndege za mafunzo za kijeshi” alisema na kuongeza
“Baada ya kuona moto ule ukizidi kushika kasi tulilazimika kuwaita wanafunzi wa Chua Cha Anga cha Kijeshi na walisaidia kwa kiwango kikubwa lakini hivi ninavyozangumza nanyi ndio tumeumaliza kuuzima wote” alisema Ndaki
Alisema chanzo cha moto huo bado hakijajulikana na maofisa uwanja wa ndege na polisi wanaendelea na uchunguzi na kusema kuwa hakuna mtu yoyote aliedhuriwa na moto huo ambao ulikuwa unakimbilia maeneo ya makazi ya watu.
Alisema kitisho kikubwa kilikuwa ni ndege za kijeshi ambazo zinakadiriwa kufikia 13 ambazo zimegesha uwanjani hapo ambazo ni za mazoezi ya kijeshi na kulazimika kutumia nguvu za ziada ili moto huo kufika eneo zilipo.
Kaimu kamanda huyo aliwashukuru wananchi wanaokaa kandokando ya uwanja huo kwa msaada wao kwa kuweza kuudhibiti moto huo pamoja na kikosi cha zimamoto  kuingia maeneo ya makazi yao.
Alisema kwa sasa huduma zote zimerudi kama kawaida ikiwa na pamoja na safari za ndege kuruka na kutua na kuviagiza vyombo vya usalama kuchunguza kwa makini tukio hilo.
                                                                         Mwisho

No comments:

Post a Comment