Saturday, January 31, 2015

REAL MADRID YAIADHIBU REAL SOCIETED

Wakicheza bila Ronaldo – hiki ndicho Madrid walichoifanya Real Societed

(null)
Ligi kuu ya Hispania maarufu kama La Liga imeendelea tena jana jioni  kwa mchezo ambao ulivihusisha vilabu vya Real Madrid na Real Sociedad.
Mchezo huo uliochezwa kwenye dimba la Santiago Bernabeu, ulikuwa ndio wa kwanza kwa kocha wa zamani wa Man United – David Moyes katika uwanja huo.
Huku wakicheza bila mshambuliaji wao tegemeo Cristiano Ronaldo ambaye amesimamishwa mechi mbili – Real Madrid  wameiadhibu Sociedad magoli 4-1.
Sociedad ndio walioanza kuziona nyavu za Madrid katika dakika ya kwanza tu ya mchezo lakini dakika mbili baadae Real walisawazisha kupitia James Rodriguez.
Ramos aliongeza lingine dakika ya 36, na Benzema akashindilia misumari ya mwisho dakika ya 51 na 76.
TIMU ZILIPANGWA HIVI
Real Madrid: Casillas, Carvajal, Varane, Ramos, Marcelo, Irrallamendi, Kroos (Khedira 81), James (Jese 74), Isco, Bale, Benzema (Hernandez 81)
Subs not used: Navas, Coentrao, Arberloa, Nacho
Scorer(s): James 3, Ramos 36, Benzema 51, 76
Booked: Irrallamendi 30, Marcelo 70, Khedira 87
Real Sociedad: Rulli, Aritz (Bergara 63), Gonzalez, Inigo Martinez, Yuri, Gorka Elustondo, Ruben Pardo, Xabi Prieto, Granero, Canales (De la Bella 46), Vela (Agirretxe 17)
Subs not used: Finnbogason, Zubikarai, Castro, Zaldúa
Scorer(s): Aritz 1,

No comments:

Post a Comment