Saturday, January 31, 2015

SHETANI AWA KIDHIBITI MAHAKAMANI

Pale ambapo jamaa wanamtaja shetani Mahakamani kwa kesi ya uhusiano wa jinsia moja…

Handcuffs_shutterstock_3
Moja ya ishu ambazo zilikuwa na mijadala mikubwa duniani mwaka 2014 ni suala la ndoa za jinsia moja, mvutano bado ni mkubwa zipo nchi ambazo ziliidhinisha na zipo ambazo zilipiga marufuku kubwa kwenye hiyo, wakapitisha na sheria kali kuzuia ikiwemo nchi ya Uganda.
Story kutoka Nigeria ni kwamba jamaa wawili Edwin Kelechi na Khulid Ibrahim wamefikishwa Mahakamani kwa kosa la kujihusisha na uhusiano wa jinsia moja.
Paul anatajwa kuwa na kosa la kumshawishi Edwin kufanya nae tendo hilo na kumuahidi kumlipa Naira 2000 ambayo ni kama 20,000 Tshs, lakini jamaa hakutimiza ahadi hiyo kitu kilichofanya wapigane na Polisi wakawakamata baadaye wakagundua kuwa walifanya kosa hilo.
Tunaomba tusamehewe kwa kosa hilo, ni shetani alitupitia… Hatutorudia kosa hilo tena,” walijitetea jamaa hao wakiwa Mahakamani, hukumu yao imetajwa kutolewa February 4, 2015.
Hakuna story itakayokupita mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia,www.tangakumekucha.blospot.com

No comments:

Post a Comment