Mkenya kwenye headlines za kunyongwa China! safari yake ilikua Nairobi – China.
Mwanadada
mwenye umri wa miaka 26 huenda akanyongwa baada ya kupatikana na hatia
ya kusafirisha dawa za kulevya nchini china ambapo Mkenya huyu Floviance
Owino, aliyehudumu kama msaidizi wa nyumbani alitiwa nguvuni May 2013
akisafiri kuelekea Beijing kutokea Nairobi.
Afisi ya ubalozi wa kenya nchini Uchina
umethibitisha kwamba huenda Floviance akanyongwa mwaka huu baada ya
kifungo chake cha miaka miwili kukamilika na haya maneno ni kwa mujibu
wa dada yake ambaye ni Judith Owino.
Judith anasema hakufahamu kuwa dada yake
alikuwa amesafiri kwenda China hadi alipopata habari kutoka
ubalozi wa kenya nchini humo.
>>Nilifahamu
kwa mara ya kwanza kuwa alikuwa China nilipopata simu kutoka kwa ofisi
za ubalozi, nlifahamu pia kwamba yuko kizuizini akisubiri kunyongwa,
ofisi ya Mashauri ya nchi za kigeni ilinipa habari kuhusu hukumu ya
kunyongwa kwa dada na kunipa kibali cha haraka kusafiri kwenda China’
Serikali ya uchina hata hivyo ilimwarifu
Judith kwamba alikuwa na muda mfupi kugeuza hukumu hiyo na kuzuia dada
yake asinyongwe, walinishauri nitafute wakili hivyo kwa sasa nahitaji
visa kwenda china maana mda unazidi kupotea.
Mpaka sasa Judith hajapata fursa ya
kuzungumza na Floviance kwani serikali ya china haikukubali hilo
lifanyike >>> ‘nilitamani sana kuongea nae lakini
walinikatalia, Floviane ana mtoto wa miaka minne aliyemuacha Kenya baada
ya kusafiri kwenda China’
No comments:
Post a Comment