Maamuzi mapya ya Kenya kwa kila abiria anaetokea Liberia.
Ugonjwa
wa Ebola ulikua tishio kubwa na stori inaongelewa sana kwenye vyombo
vya habari hata vya kimataifa miezi kadhaa iliyopita ambapo kwenye nchi
kadhaa watu wanaotokea Liberia au nchi jirani zenye ugonjwa huo walipata
tabu.
Kenya ilikua imepiga stop abiria wote
kutokea Liberia kuingia kwenye nchi hiyo ila sasa kwenye maamuzi mapya
serikali ya Uhuru imeondoa marufuku ya muda ya kutowaruhusu hao abiria,
wameruhusiwa kuingia kuanzia sasa lakini hata hivyo haimaanishi
wataingia tu bila kufanywa chochote.
Kila anaeingia kutoka Liberia na mataifa
jirani yenye ugonjwa huo wataendelea kufanyiwa uchunguzi kila wanapotua
hadi ugonjwa huo umalizike kabisa.
No comments:
Post a Comment